ELAM
CHRISTIAN HARVEST SEMINARY TANZANIA
ECHASE
SEMINARI
YA MAVUNO ELAM
P.O.Box 69
Mkwajuni Mbeya. Tel 0762532121. Email. elamseminary@gmail.com

Kuwaandaa
Watendakazi kwaajili ya Mavuno ya Nyakati za Mwisho.LUKA 10:2
MWONGOZO WA KOZI
SEMISTA YA KWANZA.
IDARA: Idara
Ya Theologia.
MSIMBO WA KOZI: EDT 100
JINA LA KOZI: Misingi ya Imani.
UKUBWA WA KOZI: Krediti 2.
I.
MAELEZO YA KOZI
Kozi hii inapitia na kutalii Misingi ya
Imani ya Kikristo. Katika kozi hii mwanafunzi atajifunza misingi mbalimbali ya imani ya Kikristo ambayo kwayo Ukristo
umejengwa. Pia kozi hii ina utathmini Ubora wa Ukristo na upee wake
ukilinganishwa na dini zingine zote. Kwa Kuwa misingi ya kitu chochote ndiyo inayotathmini ubora wa kitu hicho, hivyo
basi kozi hii inatoa changamoto kwa viongozi na watendakazi wa Kanisa katika
kuifundisha misingi ya imani kwa waamini wao na kuitetea Imani ya Kikristo kwa
uthabiti. Misingi anuai ya imani Ya
Kikristo itapitiwa na kujadiliwa kwa kina katika Kozi hii.
II. MALENGO
YA KOZI
Kozi hii inalenga kuwapa wanafunzi ujuzi
stadi na Maarifa juu ya Misingi ya imani ya Kikristo. Pia inalenga kuweka
tofauti bayana kati ya Imani ya Kikristo na imani ya dini zingine.Baada ya
Kujifunza Kozi hii mwanafunzi atakuwa na uwezo wa, Kuainisha Misingi anuai ya
Imani ya Kikristo, Kueleza upekee wa Imani ya kikristo, kuchambua na
kuitathmini Imani ya Kikristo. Pia mwanafunzi atakuwa na uwezo wa kufundisha
juu ya Misingi ya Imani ya Kikristo na
kuelezea mpango wa Mungu kwa ulimwengu mzima.
III. MAUDHUI
YA KOZI.
MADA YA 1: UFAFANUZI WA ISTILAHI.
·
Dhana ya Msingi
·
Dhana ya Imani
·
Dhana ya Ukristo
·
Dhana ya misingi ya Imani
·
Sababu za kujifunza Misingi ya Imani.
MADA YA 2: UWEPO WA MUNGU
·
Dhana ya uwepo wa Mungu
·
Njia ambazo Mungu ametumia
kujidhihirisha
·
Tabia Za Mungu
·
Sifa za Mungu
·
Utatu wa Mungu.
MADA YA 3: BIBLIA NENO LA MUNGU
LISILO NA MAKOSA.
·
Mamlaka iliyo kuu na ya mwisho katika
imani, mafundisho na mwenendo wa Imani ya Kikristo.
·
Sababu za kuiamini Biblia kuwa Neno la
Mungu.
·
Kazi ya maandiko Matakatifu.
MADA YA 4: ANGUKO LA
MWANADAMU
·
Kuumbwa kwa Mwanadamu
·
Anguko la Mwanadamu
·
Matokeo ya Anguko la Mwanadamu
·
Hitaji la wokovu kwa Mwanadamu
·
Mbingu na Jehanamu
·
Kiyama ya wafu.
·
MADA YA 5: WOKOVU KWA NEEMA KWA NJIA YA IMANI
·
Dhana ya wokovu.
·
Dhana ya Neema
·
Damu ya Yesu
ilitosha kwa ukombozi kamili.
·
Mifano ya Yesu
Kristo katika Agano la kale
·
Maandalio ya
wokovu.
MADA YA 6: KUHESABIWA
HAKI KWA NJIA YA IMANI
·
Dhana ya haki
·
Haki ya Mungu
dhidi ya mwenye dhambi
·
Upendo wa Mungu
kwa mwenye Dhambi.
·
Kukutana kwa
haki na Upendo wa Mungu dhidi ya mwenye dhambi.
MADA YA 7: KANISA
KIUMBE HAI CHA KI-MUNGU DUNIANI
·
Dhana ya kanisa
·
Aina ya makanisa
·
Kazi kuu tatu za
Kanisa.
·
Kusudi la kuwepo
kwa Kanisa.
·
Maagizo makuu ya
kanisa.
MADA YA 8: ROHO
MTAKATIFU NI MUNGU.
·
Dhana ya Roho
Mtakatifu.
·
Ushahidi wa Roho Mtakatifu kuwa ni Mungu.
·
Kazi za Roho
Mtakatifu.
·
Ujazo wa Roho Mtakatifu.
·
Umuhimu wa
Kunena kwa lugha mpya.
·
MADA YA 9 : YESU NI MUNGU
·
Ahadi ya
kuzaliwa kwa masihi
·
Kuzaliwa kwake
na Bikira
·
Ushahidi wa Yesu
Kristo kuwa ni Mungu.
·
Yesu Kristo
Mungu Kamili na Mwanadamu Kamili.
IV.
MBINU ZA UFUNDISHAJI
Kozi
itafundishwa kwa kutumia mbinu na njia
mbalimbali. Kozi itafundishwa kwa kutumia
mbinu Shirikishi ambapo mwanafunzi atakuwa mtendaji mkuu.
Baadhi ya njia zitakazotumiwa ni
Mhadhara, onesho, Majadiliano,
Semina na uwasilishaji.
V.
TATHMINI NA UPIMAJI
Kozi hii itakuwa na
Tathimini mbili, tathmini moja itakuwa ni ya mhadhili ambapo Mhadhili atawatathmini wanafunzi kupatia mazoezi na
mtihani wa mwisho wa Semista. Tathmini ya pili itakuwa ni ya wanafunzi ambapo
wanafunzi wataitathimini Kozi, Mhadhili na mwenendo mzima wa ufundishaji na Ujifunzaji
wa kozi.
Kozi hii itakuwa na mchanganuo ufuatao
wa alama
·
Jaribio la 1 alama 10
·
Jaribio la 2 alama 10
·
Kazi ya kundi alama 5
·
Kazi ya binafsi alama 10
·
Mahudhurio alama 5
·
Jumla ya Tamrini alama 40
·
Mtihani wa Seminari alama 60
·
Jumla ya alama 100.
VI. MAREJEO
Marejeo yataandaliwa na kutolewa na Mhadhiri atakaefundisha Kozi hii.
MTAALA HUU UMEANDALIWA NA KURUGENZI
YA MAADIKO NA MACHAPSHO
NOVEMBA 2015
………………………………………
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni