Jumamosi, 20 Agosti 2016

mwongozo wa kozi ya Karama za Roho Mtakatifu



 ELAM CHRISTIAN HARVEST SEMINARY TANZANIA
ECHASE
SEMINARI YA MAVUNO ELAM
P.O.Box 69 Mkwajuni Mbeya. Tel   0762532121.  Email. elamseminary@gmail.com

Kuwaandaa Watendakazi kwaajili ya Mavuno ya Nyakati za Mwisho.
LUKA 10:2


JINA LA KOZI: KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU
MSIMBO WA KOZI:  EDT 301
MHADHIRI: Rev. ERICK L.    (M. Div)

I.                   MAELEZO YA KOZI
Kozi hii ya Karama za Roho Mtakatifu  inachunguza, kuchambua na kuainisha  karama tisa (9) za kiutendaji za Roho Mtakatifu kama zinavyoelezwa katika Maandiko Matakatifu (Biblia). Inajadili namna Karama hizi  zinavyotenda kazi na namna  mwamini na kiongozi wa kanisa anavyoweza kuhudumu katika Karama za Roho Mtakatifu.  Kozi hii pia Kujadili umuhimu wa Karama za Roho Mtakatifu katika kanisa katika karne zote


II.                 MALENGO YA KOZI
Kozi hii  inalenga  kutazama zaidi  Asili, utendajikazi na matumizi ya Karama za Roho Mtakatifu kama vilivyofunuliwa na kuelezwa  katika Maandiko Matakatifu, Kutoa msimamo  wa ki-Biblia na ki-Theolojia  juu ya utekelezaji na utendaji wa Karama.  Kueleza sehemu zenye utata na mafundisho yasiyo ya ki-Biblia kuhusu karama za Roho Mtakatifu.

Baada ya kujifunza Kozi hii mwanafunzi aweze :-
v  Kueleza dhana ya Karama
v  Kufafanua dhana ya Karama za Roho Mtakatifu
v  Kueleza asili ya Karama Za Roho Mtakatifu
v  Kujadili Makusudi ya kutolewa kwa  Karama za Roho Mtakatifu
v  Kuainisha aina mbalimbali za Karama za Roho Mtakatifu
v  Kuzigawa karama za Roho Mtakatifu katika mafungu au makundi matatu
v  Kujadili kila karama namna inavyotenda kazi na namna mwamini anavyoweza kuhudumu katika karama husika.
v  Kujadili nadharia za ukomo wa ishara na miujiza katika kanisa
v  Kutathmini  utendajikazi wa ishara na maajabu katika historia ya Kanisa  tangu mwka 100  B.K hadi sasa.

III.             MAUDHUI YA KOZI  
MODULI YA KWANZA:                           ROHO MTAKATIFU
i.                    Dhana ya Roho Mtakatifu
ii.                  Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu
iii.                Ubatizo wa Roho Mtakatifu
MODULI YA PILI:                        ROHO MTAKATIFU NA MWAMINI
i.                    Roho Mtakatifu humsaidia Mwamini
ii.                  Kumpokea Roho Mtakatifu
iii.                Kunena/kusema kwa lugha

MODULI YA TATU:                 KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU
i.                     Dhana ya  Karama
ii.                  Dhana ya Karama za Roho Mtakatifu
iii.                Asili ya Karama za Roho Mtakatifu
iv.                Madhumuni/ Makusudi ya kutolewa kwa Karama za Roho Mtakatifu
v.                  Umuhimu wa Karama za Roho Mtakatifu katika Kanisa.
vi.                Nia yetu tunapohudumu katika Karama za Roho Mtakatifu.
vii.              Aina za Karama za kiutendaji za roho Mtakatifu
viii.            Makundi ya Karama za Roho Mtakatifu.

 MODULI YA NNE:                KARAMA ZA NDIMI/USEMI/UVUVIO
i.                    Dhana ya Karama za ndimi
ii.                  Karama ya aina za Lugha
a.       Dhana ya aina za lugha
b.      Namna karama ya aina za Lugha inavyotendakazi
c.       Madhumuni ya Karama ya Aina za Lugha
d.      Mwongozo wa kimatumizi wa Karama ya Aina za Lugha

iii.                Karama ya Tafsiri   za Lugha
a.       Dhana ya Tafsiri za Lugha
b.      Madhumuni ya Karama ya Tafsiri za Lugha
c.       Namna Karama ya Tafsiri za Lugha inavyotendakazi
d.      Masharti ya Karama ya Tafsiri za Lugha
e.       Mwongozo wa kimatumizi wa Karama ya Tafsiri za Lugha

iv.                Karama ya Unabii
a.       Dhana ya unabii
b.      Tofauti kati ya hudma ya nabii na Karama ya Unabii.
c.       Kusudi la Karama ya unabii
d.      Vile Karama  ya Unabii isivyo
e.       Mwongozo wa kupima Unabii
f.       Mwongozo wa kimatumizi wa Karama ya Unabii

MODULI YA TANO:                                 KARAMA ZA UFUNUO

        i.            Dhana ya Karama  za Ufunuo
      ii.            Kusudi la Karama za ufunuo
    iii.            Aina ya Karama za Ufunuo

    iv.            Karama  ya Neno la Maarifa.
a.       Fasili ya Neno la Maarifa
b.      Vile Karama ya Neno la Maarifa  isivyo.
c.       Makusudi ya Karama ya Neno la Maarifa
d.      Jinsi  Karama ya Neno la Maarifa invyotendakazi
e.       Mwongozo wa Kimatumizi/utendaji wa Karama ya Neno la Maarifa.

      v.            Karama ya Neno la Hekima
a.       Fasili ya Neno la Maarifa
b.      Vile Karama ya Neno la Hekima isivyo
c.       Uhusiano kati ya Neno la Hekima na Neno la Maarifa.
d.      Madhumuni/Makusudi ya Karama ya Neno la Hekima
e.       Namna Karama ya Neno la Hekima inavyotenda kazi
f.       Mwongozo wa kiutendaji wa Karama ya Neno  la Hekima

    vi.            Kupambanua roho.
a.       Fasili ya kupambanua roho
b.      Vile Karama  hii isivyo
c.       Madhumuni ya Karama ya Kupambanua roho
d.      Namna Karama ya Kupambanua roho  inavyotenda kazi.
e.       Mwongozo wa kiutendaji wa Karama ya Kupambanua roho.


MODULI YA SITA:                     KARAMA ZA NGUVU/ UWEZO
i.                    Fasili ya Karama za  nguvu
ii.                  Aina ya Karama za Nguvu
iii.                Madhumuni ya Karama za Nguvu.



iv.                Karama ya Imani
a.       Fasili ya Karama ya Imani
b.      Madhumuni ya Karama ya Imani
c.       Uhusiano kati ya Karama ya Imani na Karama nyingine za Nguvu
d.      Namna Karama ya Imani inavyotenda kazi
e.       Mwongozo wa Kiutendaji wa Karama ya  Imani

v.                  Karama za Uponyaji
a.       Fasili ya Karama za Uponyaji
b.      Madhumuni ya  Karama za Uponyaji
c.       Namna Karama  za Uponyaji inavyotenda kazi.
d.      Mwongozo wa kiutendaji wa Karama  za Uponyaji.

vi.                Karama ya Matendo ya Miujiza
a.       Fasili ya Mtendo ya Miujiza
b.      Madhumuni ya Karama ya Matendo ya Miujiza
c.       Namna Karama ya Matendo ya Miujiza inavyotenda kazi
d.      Mwongozo wa Kiutendaji wa Karama ya  Matendo ya Miujiza.

MODULI YA SABA:  ISHARA NA MAAJABU SIKU HIZI
i.                    Usuli
ii.                  Nadharia za Ukomo wa Ishara na Miujiza
iii.                Mapungufu ya Nadharia za Ukomo
iv.                Mawazo ya Wana-Injili wasiokubali mabadiliko.


MODULI YA NANE:          ISHARA NA MAAJABU KATIKA HISTORIA YA KANISA

i.                    Fasili ya Ishara na Maajabu
ii.                  Kipindi cha Kale  Miaka ya 100-600.  B.K
iii.                Kipindi cha Kati Miaka ya  600 -  1500 B.K
iv.                Wakati wa Matengenezo ya Kanisa Miaka ya  1500 -  2000  Wakati wa  sasa.


IV.         MBINU ZA UFUNDISHAJI
Kozi hii ina   masaa 30 ya Mihadhara na Masaa   15  ya Semina,  jumla  ina masaa 45 ya ufundishaji.  Kozi itafundishwa kwa  kutumia mbinu na njia mbalimbali. Kozi itafundishwa kwa kutumia  mbinu   Shirikishi  ambapo mwanafunzi atakuwa mtendaji mkuu. Baadhi ya njia zitakazotumiwa ni  Mhadhara, onesho, Majadiliano,   Semina na uwasilishaji.


V.           TATHMINI  NA UPIMAJI
 Kozi hii itakuwa na Tathimini mbili, tathmini moja itakuwa ni ya  mhadhili ambapo  Mhadhili  atawatathmini wanafunzi kupitia mazoezi na mtihani wa mwisho wa Semista. Tathmini ya pili itakuwa ni ya wanafunzi ambapo wanafunzi wataitathimini Kozi,  Mhadhili  na mwenendo mzima wa ufundishaji na Ujifunzaji wa kozi.
Kozi hii itakuwa na mchanganuo ufuatao wa alama
·         Jaribio la 1 alama 10
·         Jaribio la 2 alama 10
·         Kazi ya kundi alama 5
·         Kazi ya binafsi alama 10
·         Mahudhurio alama 5
·         Jumla ya Tamrini alama 40
·         Mtihani wa Seminari alama 60
·         Jumla ya alama 100.



MAREJEO


Gill,A, L (1995) Maisha ya Miujiza- ISOM Muhula wa kwanza. USA
Peter, W (1985) Your Spiritual gift can help your church grow. Kent Cox al Wyman
Rawland,G (1996)Kupokea Ubatizo wa Roho Mtakatifu na Karama zake: Fimbo ya Mchungaji.Indira Printers.New Delh 110020.
Thomas, A.P (1992) Karama za Rohoni: Jinsi Pentekoste inavyofanya kazi na kukaribia watu.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni