ELAM
CHRISTIAN HARVEST SEMINARY TANZANIA
ECHASE
SEMINARI
YA MAVUNO ELAM
P.O.Box 69
Mkwajuni Mbeya. Tel 0762532121. Emai elamseminary@gmail.com

Kuwaandaa
Watendakazi kwaajili ya Mavuno ya Nyakati za Mwisho.LUKA 10:2
MWONGOZO WA KOZI
SEMISTA YA KWANZA.
IDARA: Idara
Ya Theologia
MSIMBO WA KOZI: EDT 105
JINA LA KOZI: Bibliolojia
UKUBWA WA KOZI : Krediti 3.
I.
MAELEZO
YA KOZI
Kozi hii ya Bibliolojia
inachunguza historia ya Biblia na kuthibitisha ukweli wa Biblia kuwa Neno la
Mungu.Katika kozi hii mwanafunzi atajifunza stadi na maarifa mbalimbali yahusuyo
elimu ya Biblia. Mwanafunzi atajifunza upekee Wa Biblia na Ubora wake
ikilinganishwa na vitabu vingine vya dini, nyingine, Sayansi na Falsafa.
Katika Kozi hi
mwanafunzi atajifunza hatua mbalimbali Biblia ilizopitia tangu kuandikwa kwake hadi kuenea kwake
ulimwenguni kote. Pia Kozi hii inatazama
jinsi Biblia ilivyopambana na maadui zake na kuwashinda. Kozi hii ni kozi ya msingi katika Kozi zote za
Theologia ya Kikristo. Inasimama kama
daraja la kozi zingine za Theologia.
II.
MALENGO
YA KOZI.
Kozi hii inalenga
kumjengea mwanafunzi msingi wa kitheologia ya Kikristo ambayo kiini chake ni Biblia
Takatifu.Baada ya kujifunza Kozi hii mwanafunzi atakuwa na uwezo wa kueleza
jinsi Biblia ilivyoandikwa,lugha za Biblia, Jinsi Biblia ilivyopambana na
Maadui zake na kuwashinda kabisa. Jinsi vitabu vya Biblia vilivyokusanywa na
kuwekwa pamoja kuwa kitabu kimoja. Pia mwanafunzi ataweza kutoa ushahidi wa
Biblia kuwa Neno la Mungu na kuweza kueleza jinsi Mungu alivyohusika katika uandishi wa Biblia,
kuhifadhiwa kwake na jinsi Mungu anavyohusika sasa kwa wasomaji wa Biblia. Pia
mwanafunzi ataweza kueleza Mpango wa Mungu kwa ulimwengu zima kama Biblia
inavyofundisha. Baada ya kujifunza kozi hii mwanafunzi anatarajiwa kuwa shahidi
mwaminifu wa imani Ya ki- kristona kutetea ukweli wa Ki- Mungu siku zote za
maisha yake.
III.
MAUDHUI
YA KOZI.
MADA YA 1. USULI WA BIBLIA.
·
Asili
ya Neno-Biblia
·
Maana ya Biblia.
·
Kiini cha Biblia
·
Ujumbe wa Biblia
·
Lugha za Biblia
·
Umoja wa Biblia
·
Nyakati za kuandikwa kwa Biblia
·
Tafsiri za Biblia za Zamani sana
·
Nakala za Biblia za zamani zilizopo leo.
·
Sababu za kujifunza Biblia
MADA
YA 2. USHAHIDI WA BIBLIA KUWA NENO LA
MUNGU.
·
Uwezo wa Biblia kubadili maisha ya watu
·
Unabii uliotimizwa na unaoendelea
kutimizwa
·
Kujibiwa kwa maombi
·
Ushahidi wa uchimbuaji.
·
Umoja waBiblia.
MADA YA 3: KANUNI YA
BIBLIA
·
Dhana ya Kanuni
·
Maana ya Kanuni ya Biblia
·
Sababu za kuwa na Kanuni ya Biblia.
·
Kanuni za Biblia.
·
Vitabu vya Apokrifa.
MADA YA 4: KUENEZWA KWA
BIBLIA ULIMWENGUNI KOTE.
·
Peter Waldo
·
John Wyklif
·
Wiliam Tyndale.
·
Kutafsiriwa kwa Biblia Duniani kote.
I.
MBINU ZA UFUNDISHAJI
Kozi
itafundishwa kwa kutumia mbinu na njia
mbalimbali. Kozi itafundishwa kwa kutumia
mbinu Shirikishi ambapo mwanafunzi atakuwa mtendaji mkuu.
Baadhi ya njia zitakazotumiwa ni
Mhadhara, onesho, Majadiliano,
Semina na uwasilishaji.
II.
TATHMINI NA UPIMAJI
Kozi
hii itakuwa na Tathimini mbili, tathmini moja itakuwa ni ya mhadhili ambapo Mhadhili atawatathmini wanafunzi kupatia mazoezi na
mtihani wa mwisho wa Semista. Tathmini ya pili itakuwa ni ya wanafunzi ambapo
wanafunzi wataitathimini Kozi, Mhadhili na mwenendo mzima wa ufundishaji na Ujifunzaji
wa kozi.
Kozi hii itakuwa na mchanganuo ufuatao
wa alama
·
Jaribio la 1 alama 10
·
Jaribio la 2 alama 10
·
Kazi ya kundi alama 5
·
Kazi ya binafsi alama 10
·
Mahudhurio alama 5
·
Jumla ya Tamrini alama 40
·
Mtihani wa Seminari alama 60
·
Jumla ya alama 100.
III.
MAREJEO
Marejeo yataandaliwa na kutolewa na Mhadhiri atakaefundisha Kozi hii.
MTAALA HUU UMEANDALIWA NA KURUGENZI
YA MAADIKO NA MACHAPSHO
NOVEMBA 2015
………………………………………
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni