Jumamosi, 20 Agosti 2016

MWONGOZO WA KOZI YA UPAKO WA ROHO MTAKATIFU 2016/2017



ELAM CHRISTIAN HARVEST SEMINARY TANZANIA
ECHASE
SEMINARI YA MAVUNO ELAM
P.O.Box 69 Mkwajuni Mbeya. Tel 0762532121. Emai elamseminary@gmail.com



Kuwaandaa Watendakazi kwaajili ya Mavuno ya Nyakati za Mwisho.
LUKA 10:2

 KIHUNZI CHA KOZI

SEMISTA YA   SITA
IDARA:                                   Idara Ya  Theologia
MSIMBO WA KOZI:           ED T 606
 JINA LA KOZI :         UPAKO WA ROHO MTAKATIFU
 UKUBWA WA KOZI :       Krediti 3.

MHADHIRI: Rev. Erick .L. M
I.                  MAELEZO YA KOZI
Kozi hii ya Upako wa Roho Mtakatifu  Inapitia na kujadili kwa kina  Juu ya upako wa Roho Mtakatifu. Inachunguza, kuchambua na kuainisha jinsi Upako wa Roho Mtakatifu ulivyo na namna unavyotendakazi katika maisha ya Mwamini na viongozi na watendakazi wa kanisa. Aidha Kozi hii inachunguza kanuni mbalimbali za kupokea upako na jinsi na namna ya kufanya ili kutembea katika Upako wa Roho Mtakatifu. Kozi hii inaweka mkazo katika kuwapa changamoto waamini, Watendakazi na viongozi wa Kanisa   kutembea  na kufanya kazi ya huduma katika upako wa Roho Mtakatifu.


II.               MALENGO YA KOZI
Kozi hii  inalenga  kuwawezesha Wanafunzi kufanya kazi ya huduma katika upako wa Roho Mtakatifu.  Inalenga kuwapa hamasa viongozi, Watendakazi na Waamini  wote kwa ujumla kujihusisha katika Upako wa Roho Mtakatifu.
Baada ya kujifunza Kozi hii mwanafunzi ataweza, Kueleza dhana ya Upako wa Roho Mtakatifu, Kanuni za Upako wa Roho Matakatifuu, namna  Upako wa Roho Mtakatifu unavyotenda kazi, kweli kadhaa kuhusu Upako wa Roho Mtakatifu,  Jinsi ya kutunza Upako na namna ya kupokea upako  mara tatu. Baaada ya kujifunza Kozi hii mwanafunzi anatarajiwa kuanza kuishi, kutembea  kutenda na kufanya kazi ya Huduma kwa upako wa Roho Mtakatifu.



III.           MAUDHUI YA KOZI

MODULI YA KWANZA: UTANGULIZI WA KIHISTORIA NA KINABII JUU YA UPAKO WA ROHO MTAKATIFU.
1.     Dhana ya Upako wa Roho Mtakatifu
2.     Upako katika Agano la kale
a)     Asili ya neno Upako
b)    Asili ya neno Masihi

3.     Upako katika Agano Jipya
a)     Aleopho
b)    Chrio
c)     Charisma

MODULI YA PILI:  AILI, MAKUSUDI NA MATUMIZI YA UPAKO
A.   Asili ya Upako
B.   Kusudi la Upako
C.   Kazi ya Upako


MODULI YA TATU: KUTEMBEA KATIKA UPAKO WA ROHO MTAKATIFU
A.   Namna ya kupokea Upako wa Roho Mtakatifu
B.   Kukua katika upako wa Roho Mtakatifu
C.   Kulinda upako Wa Roho Mtakatifu
MODULI YA NNE:     KUPOKEA UPAKO MARA TATU
  Utangulizi
A.   Upako wa aina tatu
1.     Upako wa Mkoma
2.     Upako wa kuhani
3.     Upako wa Kifalme.
B.    Mifano ya Upako mara tatu
C.   Upako uliogawanyika
D.   Hitimisho
IV.       MBINU ZA UFUNDISHAJI
Kozi hii ina jumla ya masaa 30 ya ufundishaji na masaa 15 ya semina na jumla ya masaa 45 ya ujifunzaji na ufundishaji.  Kozi itafundishwa kwa  kutumia mbinu na njia mbalimbali. Kozi itafundishwa kwa kutumia  mbinu   Shirikishi  ambapo mwanafunzi atakuwa mtendaji mkuu. Baadhi ya njia zitakazotumiwa ni  Mhadhara, onesho, Majadiliano,   Semina na uwasilishaji.

V.         TATHMINI  NA UPIMAJI
 Kozi hii itakuwa na Tathimini mbili, tathmini moja itakuwa ni ya  mhadhiri  ambapo  Mhadhiri  atawatathmini wanafunzi kupitia mazoezi na mtihani wa mwisho wa Semista. Tathmini ya pili itakuwa ni ya wanafunzi ambapo wanafunzi wataitathimini Kozi,  Mhadhiri  na mwenendo mzima wa ufundishaji na Ujifunzaji wa kozi. Kila mwanafunzi anatakiwa kushiriki kikamilifu katika kujifunza na kufuata maelekezo yanayotolewa  na mhadhiri wa Kozi.
Kozi hii itakuwa na mchanganuo ufuatao wa alama
·        Jaribio la 1 alama 10
·        Jaribio la 2 alama 10
·        Kazi ya kundi alama 5
·        Kazi ya binafsi alama 10
·        Mahudhurio alama 5
·        Jumla ya Tamrini alama 40
·        Mtihani wa Seminari alama 60
·        Jumla ya alama 100.





VI.                                      MAREJEO


Mahony R,1996, Kupokea Upako mara tatu, Fimbo ya mchungaji. Kilpaul, Chennai 600 010, T.N., INDIA.
Miller, R.M () Huduma yenye Nguvu: Uhudumu katika nguvu na upako wa Roho Mtakatifu. Springfield, MO, USA
 Parrish,F, R, () Upako wa Roho Mtakatifu: (2014) Matendo: Kilpaul, Chennai 600 010, T.N., INDIA.

MTIHANI WA HISTORIA YA KANISA "I" 2016/2017



Jinala Mwanafunzi ………………………………….……….Namba Ya Usajiri…………………
ELAM CHRISTIAN HARVEST SEMINARY TANZANIA
Seminari Ya Mavuno Elam
ECHASE



Kuwaandaa Watendakazi kwaajili ya Mavuno ya Nyakati za Mwisho.
LUKA 10:2
MTIHANI WA KUHITIMU KOZI ZA MUHULA WA KWANZA2016/2017

MUDA SAA 3:00
IDARA YA THEOLOJIA
EDT 300
HISTORIA YA KANISA “I”

MAELEKEZO
·        Mtihani huu una sehemu  A, B na C
·        Jibu maswali yote kama ulivyoulizwa
·        Usipoteze muda katika swali moja usilolijua
·        Usafi ni muhimu na utazingatiwa katika utoaji alama.   Swali lililofutafutwa halitapewa alama.

SEHEMU “A” MACHAGULIO  (alama 40)
Soma maswali yafuatayo na kasha jibu kwa kujaza katika jedwali lililopo hapo chini.

1.     Kanisa la Pergamo linawakilisha kipindi cha …………..cha kanisa
a)     Kipindi cha mitume
b)    Kipindi cha mateso
c)     Kipindi cha matengenezo
d)    Kipindi cha kifahari.

2.     Mfiadini wa kwanza alikuwa ni:
a)     Paulo
b)    Musa
c)     Timotheo
d)    Stefano.




3.     Mwanzo wa  kanisa ulikuwa ni:-
a)     Antiokia
b)    Bethlehemu.
c)     Yerusalemu
d)    Nazareti.

4.     Alitawadhwa kuwa Askofu mwaka mmoja tu baada ya kuokoka.
a)     Iginasi
b)    Leonidasi
c)     Sipriani
d)    Yesu.

5.     Kanisa lilianza
a)     Goligotha
b)    Siku ya Pentekoste
c)     Kalvari
d)    Msalabani

6.     Ulijulikana kama nuru ya Asia.
a)     Tiathira
b)    Efeso
c)     Pergamo
d)    Laodekia.

7.     Mojawapo ya maadui kanisa liliokabiliana nao mara baada ya kuanza :-
a)     Wayahudi
b)    Mafasisayo
c)     Masadukayo
d)    Waeseni
8.     Wanachama  wa kanisa la kwanza walikuwa ni
Wayunani
a)     Wayahudi
b)    Wamataifa
c)     majbu yote hapo juu ni sahihi.
9.     Siku kanisa linaanza  Petro alipohubiri Waliokoka  
a)     Watu 4000
b)    Watu 3000
c)     Watu 5000
d)    Watu 10000.

10.            Walianza wakati wa kipindi cha Ezra waliporudi toka uhamishoni.
a)     Mafarisayo
b)    Waeseni
c)     Masadukayo
d)    Wayahudishaji

11.            Mkutano ulioitishwa kwaajili ya kushughulikia suala la wokovu  kwa watu wa kimataifa ikiwa walipaswa kushika Torati au la
a)     Mkutano wa Yerusalemu
b)    Mkutano wa Nikea
c)     Mkutano wa Kostantinopali
d)    Mkutano wa Efeso



12.            Mkutano wa kwanza wa kanisa zima
a)     Mkutano wa Yerusalemu
b)    Mkutano wa Nikea
c)     Mkutano wa Kostantinopali
d)    Mkutano wa Efeso

13.            Alileta uamsho mkubwa kule Samaria
a)     Tomaso
b)    Filipo
c)     Mathayo
d)    Yohana.

14.            Wasamaria walikuwa na hekalu lao huko:-
a)     Yerusalemu
b)    Bethlehemu
c)     Uyahudi
d)    Gelizimu.
15.            Hawakupatana na wayahudi.
a)     Wayunani
b)    Wayahudi
c)     Wasamaria
d)    Wainjilisti

16.            Mwamini wa kwanza katika bara la Ulaya alikuwa mwanamke aliyeitwa
a)     Dorkasi
b)    Lidia
c)     Prisila
d)    Perpetua

17.            Katika karne ya pili karibuni wanazuoni wote wa  Kikristo walifundisha kwamba Yesu alikuwa :-
a)     Theotokos
b)    Pneumatologia
c)     Logosi
d)    Rhema

18.            Watu wa ……….Waliitwa waungwana kule wale wa Thesolanike
a)     Warumi
b)    Waefeso
c)     Wakolosai
d)    Waberoya.


19.            Alimuua baba wa mwanatheolojia mkuu
a)     Nero
b)    Deokletiani
c)     Domitiani
d)    Septimus

20.            Alikuwa na miaka 16 alipoingia katika utawala
a)     Nero
b)    Deokletiani
c)     Domitiani
d)    Septimus


Swali
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
Jibu

























SEHEMU B: (alama 40) KWELI AU SIKWELI
Weka tiki  katika  jibu sahihi kutokana na ulivyojifunza katika kozi hii.
Swali
Maelezo
Hapana
Ndiyo
1.      
Deokletiani aliamuru Biblia zichomwe moto


2.      
Yustin Shahidi alikuwa askofu  wa Smirna


3.      
Leonidasi alikuwa baba wa mwanatheolojia mkuu


4.      
Shule ya  Biblia ya Alexandria ilikuwa Rumi


5.      
Klaudi  Nero alimuua Sipriani askofu wa Antiokia


6.      
Domitiani alimsulubisha Petro mnamo mwaka 90 B.K


7.      
Mkutano wa kwanza wa Yerusalemu uliitishwa mnamo mwaka 48 B.K


8.      
Yerusalemu  ilibomolewa mnamo mwaka 70.B.K


9.      
Donato aliongoza uasi  katika karne ya nne B.K


10.             
Novatiani aliongoza uasi katika karne ya tatu


11.             
Marsion alidai kwamba Injili ni kwa watu wote


12.             
Montano alidai kwamba Injili ilitegemea falsafa na mafumbo


13.             
Askofu Sextus wa Rumi ni mtu wa kwanza Kutengeneza Kanuni ya Maandiko ya Matakatifu


14.             
Askofu Polikapu alikuwa mwanafunzi wa Mtume Yohana


15.             
Origeni alikuwa mwalimu wa Theolojia


16.             
Katika karne ya pili kanisa lilipambana na maadui watatu


17.             
Kanisa lilipitia vipindi kumi vya mateso sawasawa na unabii wa kanisa la Smirna


18.             
Waraka wa Balnaba uliandikwa na mtume Paulo


19.             
Pelpetua aliuuwa kama shahidi wa imani kule Kathegi


20.             
Marsioni alianzisha Mlengo wa Umontano














SEHEMU  C  (Alama  20) MASWALI YA  KUOANISHA
Oanisha kati ya Orodha A na Orodha B kwa kujaza katika jedwali lililotolewa baada ya jedwali la maswali.
ORODHA “A”
ORODHA “B”
1.      Spriani
Alijiua mnamo mwaka 68.B.K
2.      Sextus
A.    Ulikataliwa kuingizwa kwenye Kanuni  Ya Maandiko Mt
3.      Ignasi
B.     Askofu wa Rumi
4.      Ufunuo wa Mtume Petro
C.     Aliagiza kubomolewa kwa majengo ya makanisa
5.      Polikapu
D.    Mafundisho ambayo hayakukubaliwa na kanisa
6.      Deokletiani
E.     Paulo na Balnaba
7.      Nero
F.      Marko
8.      Uzushi
G.    Askofu wa Smirna
9.      Wamishenari wakuu
H.    Askofu wa Antiokia
10.  Chanzo cha mgogoro
I.       Alipewa uaskofu mwaka mmoja baada ya kuokoka

J.       Paulo na Petro

K.    Mfia dini wa kwanza

L.     Alitawala kwa miaka 100

M.   Deusius

N.    Septimus Severus

Jedwali la majibu
Swali
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Jibu











KALENDA YA MATUKIO
Soma kwa makini maelezo na miaka na kisha jaza katika jedwali lililotolwa chini baada ya jedwali la matukio
MATUKIO
MIAKA
1.     Mkutano wa kwanza wa Kanisa zima
A.   48. B.K
2.     Nero alianza kutawala
B.   312 B.K
3.     Patano la amani la Mfalme Kostantino
C.   Karne ya tatu
4.     Kuanguka kwa dola ya Rumi
D.   254
5.     Mkutano wa Kostantinopali
E.    381 BK
6.     Leonidasi anauawa
F.    30.B.K
7.     Kupaa Mbinguni  kwa Bwana  Yesu
G.    68 B.K
8.     Simoni ndugu yake Yesu anauawa
H.   476 .B.K
9.     Nero anajiua
I.       107 .B.K
10.            Kuanza kwa utawa
J.      165 .B.K
11.            Polikapu anauawa
K.   54. B.K
12.            Origeni anakufa akiwa gerezani
L.    202 B.K
13.            Yustini shahidi anauawa
M. 155 BK
14.            Sipriani anauawa
N.   325 B.K
15.            Mkutano wa Yerusalemu
O.   1453
16.            Marsioni anahukumiwa uzushi na kutengwa na kanisa
P.    1914
17.            Kuanguka kwa Kostantinopali
Q.   144 B.K
18.            Patano la Westfalia
R.   433 B.K
19.            Mkutano wa Efeso
S.    1648
20.            Vita ya kwanza ya dunia
T.    258 B.K


Swali
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
Jibu