Jumatatu, 7 Januari 2019

MISINGI YA IMANI YA ELAM CHRISTIAN HARVEST SEMINARY


ELA M CHRISTIAN HARVEST SEMINARY  NI CHUO   cha Biblia  cha kimishenari chenye msingi wa Kipentekoste  kinachotoa mafunzo katika kuwaandaa  Watendakazi na viongozi wa Kanisa.  Kwaajili ya Mavuno ya nyakati za mwisho.  Chuo hiki kinapokea wanafunzi toka  madhehebu  yote   ya Kikristo 
Tazama  ainisho la imani hapo chini

MAELEZO YA IMANI
33.0 AINISHO LA MAELEZO YA IMANI
        i.            Wokovu, Tunaamini kwamba wokovu upo duniani na kwamba baada ya kufa, hakuna kuokoka, tunaokoka tukiwa duniani na si mbinguni.

      ii.            Uwepo wa Mungu mmoja tu aliye wa kweli, Tunaamini kwamba kuna Mungu wa kweli mmoja tu Mungu mmoja aliyejidhihirisha katika nafsi tatu ambazo ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.
    iii.            Biblia Takatifu, Tunaamini kwamba Biblia ni neno la Mungu lililovuviwa lisilo na makosa na ni ndio mamlaka ya mwisho na iliyokuu katika maisha ya mwamini.

    iv.            Anguko la mwanadamu, Tunaamini kwamba mwanadamu alianguka dhambini na dhambi inamtenga mbali na Mungu na hivyo anamhitaji mwokozi Yesu Kristo.

      v.            Wokovu kwa njia ya neema.Tunaokolewa kwa neema  kwa njia ya imani pekee.

    vi.            Ukombozi kutoka dhambini kupitia kifo cha kidhabihu cha Yesu Kristo. Tunaamini kwamba Mungu alifanyika mwili na kufa msalabani kama fidia au dhabihu ya dhambi, na kwa njia hii mwanadamu anaweza kupatanishwa na Mungu tena.

  vii.            Kanisa moja tu ulimwenguni lililo mwili wa Kristo linalowaunganisha ndani yake waamini wote wa kweli. Tunaamini kwamba Kanisa ni kiumbe hai ambacho Mungu anakitumia kuufikia ulimwengu wote.
viii.            Uwepo wa huduma tano za uongozi. Tunaamini kwamba Yesu Krisot alitoa huduma tano za uongozi ambazo ni mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu kwa kusudi la kuwaandaa watakatifu kwaajili ya huduma. Huduma  hizi zote zipo ndani ya kanisa hata sasa. Hakuna huduma iliyokuwa ya muda tu bali zote zinatenda kazi hata sasa.
    ix.            Ufufuo wa wafu, Tunaamini kuwa kuna maisha mengine baada ya kufa, Kufa ni njia tu ya kuingia katika maisha mapya ya milele, na hivyo kutakuwa na ufufuo wa wafu wote  watakatifu wataurithi uzima wa milele na waovu watatupwa katika ziwa la moto.
      x.            Tumaini la Baraka.  Tunaamini kwamba Yesu Kristo atarudi mara ya pili kulichukua kanisa yaani watakatifu na kwenda nao mbinguni.
    xi.            Uwepo wa jehanamu. Tunaamini hukumu ya waovu na mwisho wao ambao ni kutupwa katika ziwa la moto.
  xii.            Uwepo wa miujiza. Tunaamini kwamba miujiza ipo mpaka sasa ndani ya kanisa na kwamba haikuwa kwaajili ya kipindi fulani tu cha kanisa, bali ni kwa vizazi vyote mpaka Bwana Yesu atakaporudi.
xiii.            Maisha matakatifu.  Tunaamini kwamba maisha matakatifu ndio  msingi wa ukristo. Bila kuishi maisha matakatifu hakuna ukristo.
xiv.            Ukuhani wa waamini wote.  Tunaamini kwamba kila mwamini wa kweli ni kuhani, anaowajibu wa kumwendea Mungu na kusimama katika huduma.  Mungu anataka kila mwamini amtolee dhabihu za maombi, sifa na shukrani na kuzitangaza fadhili zake.




   




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni