Jumamosi, 20 Mei 2017
DHANA YA UVUVIO WA BIBLIA
MAFUNDISHO YA
BIBLIA
By .Rev. Dr Erick L Mponzi
DHANA
YA UVUVIO WA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA )
1.
Uvuvio wa Maandiko Matakatifu.
Neno la Mungu
Linanena:
Maana
unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu
walinena
yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. Petro 1:21.
Kila
Andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya
watu
makosa yao, na kwa kuwaonya, na kuwaadhibisha katika haki. Timotheo wa
pili
3:16.
I.
Maana ya Pumzi
Neno Pumzi
lililotumiwa katika Timotheo wa pili 3:16 linatokana na neno la Kigriki theo
Pheustos na linaonyesha ya kwamba Mungu (Theos) alipuzia (Pneo= kupuliza) Neno
lake katika waandishi wa maandiko. Ni jambo la kusikitisha kujua hayo kwa
maneno mawili ya Kigriki, yaliyotumiwa kwa kupumua: Peo (kupumua na fahamu) na Psucho (kupumua polepole au
bila fahamu ), Pneo linatumiwa. Pumzi,
kwa hivyo
ilikuwa ni kupuzia kwa nguvu kwa fahamu na Mungu kwa mwanadamu, ambapo
walipokea Neno takatifu la Mungu, kwa maneno mengine watu watakatifu wa Mungu wakiwezeshwa
chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu, na kwa utiifu wa kutosha kwa amri takatifu,
kwa hivyo wakazuiliwa na kosa lolote. Kwa hali hii, maandiko yote yalitolewa na
puzio
II.
Aina mbalimbali za Pumzi
Sio kila
anayedai kuamini katika pumzi ya Biblia, anaona upuzio jinzi tunavyoona sisi, puzio
la maneno au kamili. Kwa hivyo ni muhimu kwetu kutofautisha kati ya aina
mbalimbali za pumzi. Tunapotazama katika maelezo mbalimbali, itakuwa wazi ni
kwanini tunaweza tu kukubali pumzi ya maneno au kamili kama “pumzi ya Kibiblia”.
1.
Upuziomzi wa Asili
Haya maelezo
yanakataa kwamba kuna kitu ambacho si cha kawaida, au tofauti na mengine jinsi
vile Roho wa Mungu aliingia kwenye na juu ya waandishi wa maandiko. Inadai
kwamba Biblia haijapuziwa kamwe kuliko vile Shakespeare, Mohamed, au Confucius.
Conn anaonyesha
ya kwamba kulingana na maoni haya, ni akili ya mwanadamub kuliko Roho wa Mungu
ambaye aliwazuzua waandishi wa Biblia kuandika. Hakuna kitu ambacho kingekuwa
mbali na ukweli. Evans anaitikia kweli ya kwamba ikiwa hii ingekuwa tabia ya
pumzi iliyo katika waandishi wa andiko, hakuna kile kinachotuhakikishia kwamba
hawakuwa na uwezo wa kufanya makosa, kufundisha mambo yaleyale ya uwongo ya
maisha kama vile ulivyokuwa ule mwanga wa akili yamwanadamu.
2.
Upuzio usio Kamili
(1)
Wazo la Upuzo wa Fikira
Hili wazo
linatetea kwamba ni mawazo ya waandishi tu yalipuziwa bali si maneno. Kwa
hivyo, Mungu alitoa ufunuo wake kwa dokezo lisilo pangwa sawasawa, na kuliacha
kabisa kwa mwandishi kuelezea yale mawazo yaliyopulizwa. Haya yangeonyesha ya
kwamba si kila neno katika Biblia lilipulizwa. Bali Neno la Mungu lenyewe
linasisitiza umuhimu wa Neno moja (Mathayo 5:18). Wasimamizi wa wazo hili
hawataki kufungwa na mambo ya kibiblia. Wanataka kujihifadhia wenyewe uhuru wa
kutoa ufafanuzi wao wenyewe kwa maandiko. Hata
hivyo, kama si
kila neno limepulizwa, tutawezaje kuamua ni maneno gani yamepulizwa na ni yapi
ambayo hayajapulizwa? Ikiwa tu ni mambo ya Biblia yamepulizwa, inaweza kuwa
vigumu kwetu kujua mapenzi ya Mungu.
(2)
Upuzio wa Tabia na wa Kiroho
Hili jambo
linaonyesha ya kwamba ni ushauri wa kiroho na kitabia katika
maandikoumepulizwa. Kwa maneno mengine,
Mungu angewaachia waandishi matukio haya wenyewe, hakukuwa na hitaji la Mungu
kuwapuzia. Wazo kama hilo huenda lingeacha uwezekano wa Biblia kuwa na
masimulizi na makosa mengine. Kama hatuwezi kujua kikamilifu kuhusu matukio ya
historia, tutakuwaje na uhakika juu ya ukweli wa kiroho? Kwa hivyo, waandishi
walihitajika wapulizwe wanaponakili mambo ya historia. Pache yuko sawa
anapoelezea ya kuwa shahidi ambaye haaminiwi katika njia moja hawezi kuaminiwa
katika njia nyingine yoyote.
(3)
Upuzio wa Kerygma
Wasomi wengi wanashikilia wazo hili, ambalo linadhibitisha
ya kwamba Biblia ina hadithi, mikasa na hadithi za kubuni. Ila wanasema ya
kwamba haiwazuii kuamini katika Neno la Mungu, katika njia zao wenyewe.
Kulingana na kuhitimu wazo lao hakuna mtu aliyeelimika na kuhitimu
atakayekubali kwamba Biblia imepulizwa kikamilifu. Mojawapo wa wanathiolojia
wenye himizo miongoni mwao akiwemo Rudolf Bultman, ambaye alihitimu kuvua
Biblia miujiza yote na mambo
yasiyo ya asili.
alijaribu kupunguza upuzio kwa Kerygma au mafundisho ya Biblia.Lakini
haya yangemaanisha
kwamba Kuwepo
kwa kwanza kwa Kristo
Kuzaliwa kwa
Bikira
Uungu wa Kristo
Miujiza ya
Kristo
Msamaha wa
Kristo
Ufufuo wa Kristo
Kurudi kwa
shangwe kwa Kristo
kama vile hukumu
ya mwisho, kuwepo kwa roho wazuri na wabaya, nguvu na ubinafsi wa Roho
Mtakatifu n.k. haungekuwa kweli. Ikiwa hivi ndivyo ilivyokuwa, ni kwa nini
tunaamini mafundisho ya kitabu chenye maneno kuhusu miujiza, ambayo ni yenye
udanganyifu mtupu.
3.
Upuzio wa Kutumia Nguvu
Roho Mtakatifu,
kulingana na wazo hili, alitumia waandishi wa maandiko kama mashini kuliko
watu. Biblia iliamrishwa (somwa) kwa waandishi ili kwamba chochote
walichoandika kilikuwa bila kosa. Hakuna nafasi iliyoachwa kwa maoni ya binafsi.
Wazo kama hilo lingeonyesha ya kwamba kila kitabu katika Biblia
kimeandikwa
katika mtindo mmoja, kwa sababu Mungu ndiye mwandishi wa mwisho, lakini kwamba
alitoa Neno lake kupitia kwa upuzio kwa
mwanadamu wa asili, akiwakubali kuhifadhi mtindo wao wa kuandika na ubinafsi.
Tunaamini ya
kwamba kila Neno katika Maandiko linatoka kwa Mungu. Lakini vilevile
linaonyesha mguso wa mwandishi binadamu. Unaposoma Biblia utatambua juhudi ya
kuchoma ya Paulo, utakatifu mpole wa Yohana au fikira za upole za Yakobo. Jambo
ya kwamba mwandishi alizuiliwa kutokana na makosa yote halimaanishi ya kwamba alipoteza utu wake wa
mwanzoni.
4.
Kamili, Ikijawa na Pumzi ya Maneno
Tunaposema
kwamba tunaamini katika pumzi ya maneno (kamili) ya Biblia, tunadhibitisha ya
kwamba Roho Mtakatifu aliwaongoza waandishi wa maandiko katika njia fulani,
kwamba, aliwaacha na ubinafsi wao na mtindo, ili hali akiwazuia kutokana na
makosa yote.
Upuzio wote
unamaanisha ya kwamba upuzio ni kamili na bila chochote kuachwa!
Maandiko
yanashuhudia kwa himizo hilo yanapoelezea ya kwamba “maandiko yote yanatolewa
na Mungu” (Timotheo wa pili 3:16). Kila neno (lililonenwa) katika Biblia
limepulizwa na Mungu. Baneroft anaelezea hivi: “ingawaje Roho Mtakatifu hakuchagua
maneno kwa waandishi, ni dhahiri kwamba aliyachagua kupitia kwa
waandishi. Mbali na jambo ya kwamba Andiko limepulizwa
kikamilifu kwa maneno, hata hivyo, lina historia, na lugha ya wanadamu, hata na
watenda dhambi. Katika kitabu cha Ayubu hatupati tu maneno yaliyoongelewa na
Mungu, maongezi ya Ayubu na marafiki
zake, bali hata na shetani. Kwa sababu hiyo, ni maneno tu yaliyo
zungumzwa na Mungu yalikuwa matakatifu, bali kila neno ambalo
mwandishi wa Ayubu alinakili chini ya Upuzio Mtakatifu. Kwa hivyo, kila neno
lilipulizwa na Mungu. Baada ya kutambua ni nini maana ya Upuzio wa maneno, tunaweza
sasa kuitikia Biblia kwa njia mpya. Kwa kila muumini aliyezaliwa mara ya pili,
ni hakika. Tunaposoma ukurasa mgumu na huku kuelewa, hatutairejea kama
mwanafunzi mkarimu
afanyavyo
anayesema: “kuna kitu kibaya na kifungu hiki cha andiko.” Lakini badala yake
tutasema: “kuna kasoro na kuelewa kwangu kwa kifungu hiki” na tutamuuliza Mungu
kutusaidia katika kuelewa kwetu.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)