Jumanne, 31 Machi 2015

makusudi ya kanisa



SURA YA KWANZA
MAKUSUDI YA KUWEPO KWA KANISA DUNIANI

KANISA LINALOSHIKAMANA NA MAPIGO YA MOYO WA MUNGU
Kanisa linaloshikamana na mapigo ya moyo wa Mungu ni kanisa lililozaliwa moyoni mwake na linatembea na kuishi kwenye moyo wa Mungu.
Makanisa mengi yamezaliwa kwenye mioyo ya maaskofu, mitume, manabii, madhehebu na yanatembea ndani ya mioyo yao na sio moyo wa Mungu.

Neno kanisa kwa lugha ya Kiyunani linatafsiriwa kama Ecclesia maana yake waliotwa na mfalme. Ilikuwa ni desturi kwa wayunani kwa mfalme kufanya kikao na watu wake. Na kikao hiki cha mfalme na wale walioitwa ili wasikie toka kwa mfalme na mfalme asikie kutoka kwao.Mkutano huu uliitwa Ecclesia.
Kwa hiyo kanisa ni kundi la watu walioitwa na mfalme Yesu ili wasikie kutoka kwake na yeye asikie kutoka kwao.

MAMBO YA KUFAHAMU ILI UWE KANISA LINALOSHIKAMANA NA MAPIGO YA MOYO WA MUNGU.

Ø Yesu ndio anaejenga kanisa lake.
Mathayo 16:18 “Nami nakwambia wewe ndio Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu wala milango ya kuzimu haitalishinda
Kanisa linaloshikamana na mapigo ya moyo wa Mungu ni kanisa linalojengwa na Yesu mweyewe.
  Makanisa mengi yamejengwa na watu na  taasisi na sio Yesu aliejenga makanisa hayo, hivyo hutembea na malengo yao na sio malengo ya Yesu kujenga kanisa lake.
Yesu hutumia watu aliowaita mwenyewe kujenga kanisa lake, yeye hushuka na kukaa ndani ya watu hao na kuanza kujenga kanisa lake.
1 Wakorintho 3:10-14. Kwa kadri ya neema ya Mungu niliyopewa  mimi kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima naliuweka msingi”

Ø  Kanisa ni mwili wakristo
    1koritho 12: 27 “Bali ninyi mmekuwa mwili wa kristo na viungo kila kimoja peke yake”
Kanisa kama mwili wa Kristo, unatakiwa mwili wote uwe salama. Kama kuna kiungo kimoja kina shida mwili wote hauwezi kuwa salama. Hivyo kila kiungo kina umuhimu wake kuwa salama kwa afya ya mwili wote. Mfano mfumo wa damu, uti wa mgongo, ubongo, mfumo wa upumuaji, tumbo la usagaji wa chakula. Kimoja kati ya hivyo kikisumbua mwili wote husumbua maana Mungu aliweka vyote kwa makusudi.

Mungu ameliweka kanisa kwa makusudi yake. Makusudi ya kanisa ndio yanayolifanya kanisa liwepo na liwe na afya na kukua, na kama makusudi hayo  yakafanywa yote na Moja likapungua basi afya ya kanisa itateteleka.

Ø Kutambua kuhusu AMRI KUU na AGIZO KUU. Katika agano jipya.
Ndani ya amri kuu tunapata makusudi mawili ya kanisa kuwepo duniani na ndani ya agizo kuu tunapata mambo au makusudi matatu ya kanisa kuwepo.

Mathayo 22:36-40 “Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu”? Akamwambi “mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote. Hii ndio amri iliyo kuu  tena ni ya kwanza nayapili yafanana nayo  ni  hii mpende jirani yako kama nafsi yako katika amri hizi hutegemea torati yote na manabii

Biblia yote imefupishwa katika kifungu hiki cha maandiko, hivyo ni lazima kanisa litembee katika kifungu hiki. Likifanya hivyo litakuwa limetembea sawasawa na Biblia.
                                                                                                                 
Ø Katika amri kuu tunapata makusudi makuu mawili ya kanisa kuwepo ambayo ni:-
                i.          Kuabudu. Kuabudu ni kuonesha upendo kwa Mungu, lengo la kwanza la kanisa ni kupeleka sifa kwa Mungu. Na huku ndio kumpenda Mungu kwa moyo wote (Mathayo 22:27)

              ii.           Huduma Matyho 22 :29 “Mpende jirani yako kama nafsi yako”

Waefeso 4 :12,  “Kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa kristo ujengwe”

Kusudi la kanisa tunalolipata katika amri kuu ni kuwakamilisha watakatifu ili wafanye huduma, Mtakatifu bila kujua vipawa vyake na huduma yake ndani ya kanisa na jamii anakuwa hajakamilika.
 Hayo ndio makusudi mawili ya kanisa tunayoyapata katika amri kuu.

Ø Makusudi matatu tunayoyapata katika agizo kuu ni
Mathayo 28:19-20.
Basi enendeni  mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jia la baba na Mwana na Roho Mtakatifu na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi. Tazama mimi nipo pamoja nayi hata ukamilifu wa dahari”.
Katika agizo kuu pia tunapata makusudi matatu ya kanisa ambayo ni :-
Uinjilisti, ushirika na uanafunzi.
Ø Hivyo makusudi  matano ya kanisa linalogusa moyo wa Mungu ni
      i.          Kuabudu
    ii.          Huduma
  iii.          Uinjilisti
  iv.          Ushirika
    v.          Uanafunzi

Yohana 17:4-15 “Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
Ø Kusudi la kwanza kuabudu.( 17:4)
Ø Kusudi la pili Uinjilisti (17:6)
Ø Kusudi la tatuUinjilisti (17:8)
Ø Kusudi lanneUshirika (17:12)
Ø Kusudi la tano Huduma (17:13-15)

Matendo ya mitume 2:41-47.
Hapa napo tunaona kanisa la kwanza likitembea nahayo makusudi matano ya kanisa kuwepo duniani.   Waefeso 4:11-16



KUKUA KWA KANISA
Katika kipengere hiki tutaangalia kwa upana kuhusiana na mambo matatu yaliyopo ndani ya agizo kuu ambayo ni uinjilisti, uanafunzi na ushirika.
 Mathayo 28:19-20
Basi enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho mtakatifu na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi. Tazama mimi nipo pamoja nanyi siku zote hata ukamilifu wa dahari”.

Mwanafunzi ni mtu anaeingia darasan ili ajifunze siku kwa siku na hatua kwa hatua.  Kwa hiyo kanisa ni kundi la wanafunzi wa Yesu wanaojifunza kuyashika na kuyatii mambo yote aliyoyaagiza Yesu hatua kwa hatua na siku kwa siku.
Kwa maneno mengine tunaweza kueleza kwamba kanisa ni shule ya kiungu.

Kuna mambo mengi yanayofanya shule kuwa na ubora. Baadhi ya mambo hayo ni
Uwepo wa walimu bora, ubora wa elimu, matunda ya elimu inayotolewa na wingi wa wanafunzi.
Hivyo kanisa lenye ubora pia ni kanisa lenye wanafunzi wengi wa Yesu Kristo wakiwa mahali pamoja kujifunza na kutii mambo yote aliyowaamuru Yesu. Hivyo kanisa lenye idadi kubwa ya wanafunzi ni mpango wa Mungu. Ni mojawapo ya ufanisi wa shule ya Yesu. Hivyo ni mapenzi ya Mungu tuwe wengi kanisani.

Kanisa lenye watu wengi maana yake ni watu wengi wamesamehewa dhambi, watu wengi wanakwenda mbinguni, Unjilisti mwingi umefanyika, sifa nyingi zina mwendea Mungu.

Mifano ya mikusanyiko ya kanisa la mahali  pamoja katika Biblia.
      i.          Kanisa la jangwani.
Matendo ya Mitume 7:38 “Yeye ndiye aliyekuwa katika kanisa jangwani pamoja na Yule malaika aliyesema nae katika mlima Sinai, tena pamoja na baba zetu, ndiye aliyepokea maneno ya uzima atupe sisi”
Wana wa Israeli ndio waliokuwa kanisa la jangwani, pamoja na mchungaji wao Musa
Ø Je Kanisa la jangwani lilikuwa na watu wangapi ? 
Kutoka 12:37 “Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramasesi mpaka Sukothi wapata hesabu yao kama watu mia sita elfu watu waume waliokwenda kwa miguu bila kuwahesabu watoto

    ii.          Kanisa wakati wa Yesu:-
1Petro 2:21 “Kwa sababu ndio mlioitiwa kwa maana Kristo nae aliteswa kwaajili yenu akawaachia kielelezo mfuate nyayo zake”
Hivyo Yesu ndio  kielelezo chetu ambaye tunatakiwa kumfuata vile alivyofanya.

 Luka 12:1 “Wakati huo makutano walipokutanika elfuelfu hata wakakanyagana alianza kuwaambia wanafunzi wake kwamba jilindeni na chachu ya mafalisayo ambayo ni unafiki”
Kwenye huduma ya Yesu walikusanyika maelfu ya watu na sio mamia ya watu.

Mathayo 14:21 “Nao waliokula walikuwa wanaue wapata elfu tano bila wanawake na watoto”


   iii.          Kanisa wakati wa mitume
Marko 3:13-19 Yesu aliwatuma wanafunzi 12
Luka 10:1  Baada ya huduma kuongezeka akawatuma wengine sabini.

Matendo ya mitume 2:41 “ Nao waliolipokea lile neno lake wakabatizwa na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu”

Matendo ya mitume 4:4 “lakini wengi katika hao waliolisikia lile Neno waliamini na hesabu yao watu wanaume ikawa kama elfu tano”

Matendo ya mitume16:3 “Makanisa yakatiwa nguvu katika ile imani hesabu yao ikaongezeka kila siku.
 Kumbe kanisa lenye idadi kubwa ya wanafunzi ni moja ya sifa ya kanisa linaloshikamana na mapigo ya moyo wa Mungu.












SURA YA TATU
NAMNA YA KUJENGA KANISALINALOSHIKAMANA NA MAPIGO  YA MOYO WA MUNGU

A.   NIA YA KRISTO
Kuna mambo mengi yanayoweza kukuwezesha kujenga kanisa linaloshikamana na mapigo ya moyo wa Mungu. Baadhi ya mambo hayo ni:-

1.     kubadili nia yako na mtazamo wako
 Mtazamo ni mawazo yako binafsi kuelekea  jambo fulani ,mtazamo ni jinsi unavyoyaangalia mambo au jinsi unavyoyachukulia mambo, unavyoyatafsiri mambo na kuyapa majina husika. Mtazamo ni hukumu yako binafsi kuelekea jambo fulani, mtazamo wako juu ya jambo fulani waweza kukujenga au kubomoa, ukibomoka au kuharibiwa kwa jinsi hii utakuwa haukubomolewa na shetani   bali mtazamo wako umekubomoa.
  
Kwahiyo ili kujenga kanisa linalompendeza Mungu lazima ubadili nia na mtazamo wako kuhusu kanisa na kuyakataa mapokeo yote uliyoyapokea na yakaweka mizizi ndani ya ufahamu wako lakini sio ya ki-Biblia.
Wafilipi 2:5 “Iweni na nia hiyohiyo ndani yenu,ambayo ilikuwemo ndani ya Kristo Yesu”
 Unatakiwa kuwa na nia iliyokuwa ndani ya kristo. Achana na nia za wanadamu

Wakoritho2:16 “ni nani aliyefahamu nia ya Bwana amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo”
 Ili uwe kanisa linalompendeza Mungu lazim ujue nia na mtazamo wa kristo na vikae ndani yako daima.

Ø NIA YA KRISTO NI IPI ?
   Neno nia limetafsiriwa kama idara ya fikra au mawazo ndani ya mwanadamu. hivyo kubadili nia ni kubadili namna ya kufikiri,lazima tuwe na nia ya kristo ambayo ni
i.                Nia ya kristo ni kuwa hapendi mtu yoyote apotee bali wote waifikie toba
1Petro3:9 “Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake kama wengine wanavyokudhania kukawia bali huvumilia kwenu, maana hapend mtu yeyote apotee bali wote wafikilie toba”
Watu wote kwenye mtaa, kijijini kwako,ofisini, shuleni,kazini, ukoo wako hataki hata mmoja apotee.

ii.               Ni nia na mtazamo wa kristo kuwataka watu wote waokolewe 1Timotheo 2:3-4 “hili nalo ni zuri lakubarika mbele za Mungu mwokozi wetu ambaye hutaka watu wote waokolewe na kupata kujua yaliyokweli”
  Vaa nia na mtazamo huu kwamba Mungu anataka kila unayemwona lazima aokolewe ndio yawe maombi yako na juhudi yako.

iii.            Nia na mtazamo wa Yesu anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu Matendo ya mitume 17:30 “basi zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu”
Maombi yako watu wote wa mji wako wanaokuzunguka waamuru wapate kutubu.
iv.            Ni nia na mtazamo wa Mungu kwamba neema yake ya wokovu imefunuliwa kwa wanadamu wote.
Tito 2:11 “maana neema ya mungu iwaokowayo wanadamu wote imefunuliwa
Haijalishi watu wako vibaya kiasi gani wewe fahamu tu neema ya Mungu imefunuliwa kwa wote.

v.              Nia na mtazamo wa Mungu ni kwamba jehanamu ya moto haikuandaliwa kwaajili ya watu, ameandaliwa shetani na malaika zake.
Mathayo25:41 “kisha atawaambia wale walioko mkono wa kushoto,ondokeni kwangu mliolaaniwa mwende katika moto wa milele uliowekwa tayari kwaajili ya ibilisi na malaika zake”
 
vi.            Nia na mtazamo wa kristo ni kwamba katika kristo wote watahuishwa.
 Wakorintho 15:22 “kwakuwa kama katika Adamu wote wanakufa kadharika katika kristo wote watahuishwa”

vii.           Ni nia ya Kristo kwamba mkutano mkubwa sana usioweza kuhesabika ,watu wa kila taifa   na kabila,jamaa na lugha wasimame mbele ya kiti cha enzi na mbele ya mwanakondoo wamevikwa mavazi meupe na  matawi ya mitende mikononi mwao. (Ufunuo wa Yohana7:9)



B.   KUWA NA AFYA YA KUZAA.                                                                            
Baada ya kuangalia nia ya Kristo  ni ipi na mtazamo wake, umebadilika kinachotakiwa ni kuwa na afya ili   uweze kuzaa watoto wenye afya. Fahamu kwamba Mzazi mwenye afya bora huzaa mtoto mwenye afya nzuri, na kama afya ya mzazi ni mbaya wazazi hushauliwa kushughulikia afya zao kabla ya kuzaa.
Hivyo ni muhimu kuwa na kanisa lenye afya ambalo litazaa wanafunzi wenye afya.

Biblia inazungumzia sana habari za ujenzi wa kanisa ukifananishwa na ujenzi wa nyumba1Timotheo 3:15
Kila ujenzi unagharama zake, Luka14:28-30 “Maana ninani katika ninyi kama akitaka kujenga mnara asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama kwamba anavyo vya kumalizia, asije akashindwa kuumalizia baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki wakisema mtu huyu alianza kujenga akawa hana nguvu za kumalizia.”
 Tangu unapoanza kujenga ni lazima ujue ukubwa wa nyumba unayotaka kujenga ili uweke msingi na nguzo zinazofanana na ukubwa wa jengo.

Katika kanisa msingi wake ninini? Mathayo 7:14 “msingi wa mwamba na mchanga
Ø Asikiae Neno na kutenda ni mwamba
Ø Asikiae Neno bila kutenda ni mchanga.
Neno la Mungu ni mwamba wa kanisa, ni lazima kanisa lijengwe katika msingi wa Neno.
Mathayo 16:18  Nami nakuambia kwamba wewe ndio Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu wala milango ya kuzimu haitalishinda”

1Wakorintho 3:11-13“Maana hakuna  mtu awezae kuweka msingi mwingine isipokuwa uliowekwa yaani Krsto Yesu”

Maana ya pili ya msingi wa Kanisa ni wale washirika unaoanza kanisa pamoja nao.
Ø Usimchukue kiongozi wa kanisa lingine na kumfanya kuwa kiongozi katika kanisa lako, haijalishi ni mzuri kiasi gani, baadae atakusumbua tu.
Ø Anza kanisa na watu wasio na msingi wowote, yaani wametoka dhambini.
Ø Ukimchukua kiongozi wa kanisa lingine na kumfanya kuwa kiongozi katika kanisa lako bila kumfundisha, ujue unajenga kwenye msingi wa mtu mwingine.

Warumi 15:20 “kadharika nikijitahidi kuhubiri Injili nisihubiri hapoambapo jina la kristo limekwisha tajwa, nisije ikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine”

Ø Ni salama kuanza na wanafunzi wako mwenyewe usichukue watu kutoka katika kanisa lingine na kuanza nao.
Ø Ikitokea mtu ametoka katika kanisa lingine lazima awe tayari kufundishwa upya.
Baadhi ya Wanafunzi wa Yesu walikuwa ni wanafunzi wa Yohana Mbatizaji, walipoingia kwenye huduma ya Yesu walifundishwa kwa upya kwa miaka mitatu na nusu.

Yohana 1: 35 Wanafunzi wawili wa Yohana wakamfuata Yesu, kwa hiyo msingi wa kanisa ni kuanza na NENO na WANAFUNZI WAKO.

Katika ujenzi baada ya kuimarisha msingi kutatakiwa kuimarisha nguzo.
Katika KANISA NGUZO NININI ?

Mithali 9:1 “Hekima ameijenga nyumba yake, amezichonga nguzo zake saba”
Hekima ni Yesu 1Wakorintho 1:24 “nguvu ya Mungu na Hekima ya Mungu”
Nyumba ni kanisa nguzo ni viongozi

Wagalatia 3:9  “ Tena walipokwisha kuijua neema niliyopewa , Yakobo kefa na Petro wenye sifa ya kuwa ni nguzo walinipa mimi na Balnaba mkono wa kuume wa shirika ili sisi twende kwa mataifa na wao waende kwa watu wa tohara”

Yesu alianza na viongozi 12 Marko 3:13-19  
Huduma ilipoongozeka akaweka wengine 70 Luka 10:1
Mpaka Yesu anaondoka duniani  aliacha watendakazi 500.

1Wakritho15:16 Baadae aliwatokea ndugu zaidi ya 500
Matendo 1:15 Watu120 ndio walisubiri Ujazo wa Roho Mtakatifu.

Nguzo ndio husababisha afya ya kanisa na husababisha kuzaa watoto wenye afya kizazi  hadi kizazi.
 Baada ya kuweka msingi, nguzo na hekima kinachofuata ni kuambatana au ushirika kati ya hekima, nguzo na mawe.

Ushirika tunapata katika agizo kuu kwa namna ya kuambatana Waefeso 4:1-6
Kuambatana maana yake ni shikana, gandamana, ng’ang’aniana bila kuachana.
Kuambatana ni kutoka kwenye hali ya kuwa vitu viwili, vitatu, vine na kuwa kitu kimoja.
Ø Mwanzo 2:24  Ataambatana na mkewe
Ø Mwanzo 34:3 “ Moyo wake ukaambataa na Dina
Ø Ruth 1:14 Akaambatana nae
Ø 1Samweli 18:1 “Roho ya Yonathani ikaambatana na roho ya Daudi
Ø 2Samweli 20:2 “Mkono wake ukaambatana
Ø Mathayo 19:5 na Waefeso 5:13 “ kuambatana mke na mme


C.   SILAHA KUBWA ANAYOTUMIA SHETANI KUONDOA AFYA YA KANISA
      i.          Kuondoa roho ya ushirika, umoja na kuambatana.
    ii.          Kushambulia kutoka ndani ili wale wa ndani wafungue mlango wa nje waingie.
  iii.          Shetani anayetoka nje hana nguvu ikiwa hatapewa ruhusa ya kuingia Yohana 14:30 “Yuaja mkuu wa ulimweng lakini hana kitu kwangu

Kama umekaa vizuri na Bwana shetani kutoka nje hawezi kukushambulia na kukushinda. Yesu alishambuliwa kwa kupitia mwanafunzi wake Yuda Iskariote Luka 22:3,   Mathayo 10:36

D. NAMNA YA KUONDOA VITA YA NDANI.
Kuna mbinu mbalimbali ambazo zaweza kutumika katika kuimaliza vita ya ndani, baadhi ya mbinu hizo ni:-
i.                Kumwondoa wakala wa vita aliyendani.
Mithali 22:10 “ Mtupe nje mwenye dharau na fitina itakoma”
Tito 3:10 “ Mtu mzushi umkatae”

Asiyeambatana na kiongozi ni adui wa kiongozi. Hakuna kuwa katikati Mathayo 12:30  Asiye pamoja nami yu Kinyume changu”
Washirika wanapoambatana na mchungaji upendo unajaa kanisani na Yesu anatukuzwa sana.
Yohana 13:35 “Pendaneni ninyi kwa ninyi”

Kwa kawaida kondoo hunywa  maji yaliyotulia na sio yenye mawimbimawimbi Zaburi 23:2
Uinjilisti huwa na mafanikio kama wanafunzi watambatana na kiongozi mkuu.
Ø Mathayo 15:30 “wakamwendea makutano mengi  wakamletea viwete, vipofu,mabubu,  vilema na wengine wengi wakawaweka miguuni pake akawaponya hata ule mkutano wakastaajabu walipowaona mabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanakwenda, vipofu wanaona wakamtukuza Mungu wa Israeli”

Ø Marko 2:4 “ na walipokuwa hawawezi kumkaribia kwa sababu ya makutano walitoboa dari pale alipokuwapo”
Ø Luka 22:28-29  “Walidumu pamoja nami hata   wakati wa majaribu”

E.  HATUA SABA ZA MTU ALIYEACHA KUAMBATANA AU KUELEKEA UASI.
Kuna dalili nyingi ambazo huonesha kwamba mtu huyu anaelekea kuasi au tayari kaasi. Unaweza kumtambua mtu anaeelekea kuasi kwa kuchunguza  mambo yafuatayo:-
1.    ROHO YA KUJIPANGIA AU KUTENDA KAMA APENDAVYO,
Anatii yale anayoyaona yeye kuwa ni ya muhimu
2Samweli 3:20-21 “Daudi alimsamehe Abneri lakini Yoabu akamfuata na kumuua njiani”
2 Samweli 3:26-27
Huwa hawaondoki ila wanajipangia wenyewe.

2.    KUJIKWAA NA KUKWAZIKA.
Mathayo 24:10 “ ndipo wengi watakapo jikwaa na watasalitiana na kuchukiana”
 Anakuwa mtu wa kukwazika mara kwa mara, hata  mambo ambayo zamani yalikuwa hayamkwazi sasa   yanaanza kumkwaza.

Luka 17:1 “Jifunze kusamehe maana makwazo hayana budi kuja
Kujikwaa na kukwazika hufungua mlango wa chuki, watu wenye majeraha ni rahisi kuwa waasi”
Mfano ABSALOMU
                          i.          Alikuwa na mejeraha yasiyopona juu ya dada yake Tamari kubwaka na kaka yake Amnoni 2Samweli 13:1 -22
                        ii.          Baba yake(Daudi) hakuchukua hatua yoyote 2Samweli 13:21  aliishia kukasirika bila ya kuchukua hatua yoyote sawaswa na  Mambo ya Walawi 20:17.  Adhabu yake:-

3.    KUTOJIHUSISHA  NA LOLOTE.
Anaacha kuja kwenye maombi na kazi za kanisa. (Yeremia 48:10)
Hahusiki kufanya lolote, anabaki kukosoa tu wanayofanya wengine.

4.    KUKOSOA.
Anaacha kujihusisha badala yake anaanza kuona makosa na kuyakuza.
Anaaza kuona makosa kweye Neno linavyohubiriwa.
Ataona makosa kwenye utaratibu wa ibada, jinsi jengo lilivyo na utaratibu wa ibada.
Miriamu alianza kumkosoa Musa Hesabu 12:1 “kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa”
Absalomu alianza kuyaona makosa ya uongozi wa Daudi (2Samweli 15:3)
5.    HATUA YA KISIASA
Kuwahusisha wengine kwenye mambo yako na malalmiko yako.
(2 Samweli 15:3)  “Mchungaji wetu mzuri lakini hashauriki hebu tumuombee “
Watu wasioambatana na kiongozi hupenda kushirikisha wengine mapungufu ya kiongozi wao.

Maswali yao ;
Ø Umeonaje ibada ya leo ?
Ø Unajua haijachangamka sana eti !
Ø Wengi wanahama hivi ni kwanini ?
Ø Mchungaji anaendeleaje ? anajibu yupo tu .
Ø Kanisa linaendeleaje ? anajibu lipo tu.

Ukichelewa kumwondoa Absalomu utasikia anakwenda Hebroni kuondoa nadhiri (2 Samweli 15:7-10)
Mshauri mkuu nae wa Daudi akajiunga na Absalomu (2 Samweli 15:12)
Ahithoferi mshauri wa Daudi akawa mshauri wa Absalomu (2Samweli 16:23)

6.    KUDANGANYIKA
Yohana 8:44  Shetani ni baba wa uongo
Unaweza kuwa na watu wengi wa kukutia moyo, maarifa au ujuzi na uwezo wa hayo ndio yanayoweza kukudanganya na ukawa mwasi.

Yohana 14:12 “ Utafanya kazi kubwa kuliko hizi”
Ni kweli Mungu anaweza kukutumia sana lakin usidanganyike.
Yohana 13:16 “ Amini amini nawambia ninyi mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake wala mtumwa si mkubwa kuliko aliyempeleka”
Usimdharau mwalimu wako hata siku moja kwa kudanganywa na mafanikio fulani fulani uliyoyafikia.
Shetani alijidanganya alisahau uzuri aliokuwa nao kuwa ulitoka kwa Bwana Ezekieli 28:12-17
Kujidangaya zaidi ni pale ambapo  muasi anaona kuwa anaweza kummaliza baba yake wa kiroh kwa maneno ya dini au uvumi wa uongo. Uvumi wa uongo ni hatari sana.
Mithali 30 :7 “ mwana amdharauye baba au mamaye  kunguru ataling’oa jicho lake



7.    UASI WA WAZIWAZI.
 Ni hatua ambapo wale waliodanganywa wanaanza kupambana moja kwa moja na mamlaka.  Ufunuo wa Yohana 12:4 “ na mkia wake wakokota theruthi ya nyota  za Mbinguni”
Ufunuo wa Yohana 1: 20 “ zile nyota ni malaika saba”

                i.          Shetani aliasi waziwazi kinyume cha Mungu (Ufunuo 7:12)
              ii.          Absalomu akapambana na baba yake
2Samweli 16:11 “Angalieni huyu mwanangu aliyetoka katika viuno vyangu anatafuta uhai wangu”
            iii.          Absalomu akachukua nafasi ya baba yake mpaka kitandani (2 Samweli 16: 22)
             iv.          Yuda kumsaliti Yesu(Mathayo 26:47-48)
               v.          Kora,Dathani na Abiramu na viongozi wengine 250 waliasi waziwazi kinyume cha Musa. (Hesabu 16:)

F.   HUKUMU YA UASI
Mwisho wa waasi huwa ni mmoja na wa aina moja.
 1 Samweli 15:11, “Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, kuasi ni kama ukafiri na vinyago.  Kwa kuwa umelikataa Neno la Bwana yeye nae amekukataa usiwe mfalme”
Kama kuasi ni sawa na dhambi ya uchawi Maandiko yanaagiza kwamba usimwache mchawi kuishi.
Mungu haungi mkono uasi wa aina yoyote ile
2 Samweli 15:11 “ na watu walioalikwa wakafika Yerusaleu pamoja na Absalomu wakaenda katika ujinga wao wasijue lolote

Ø Shetani Ufuo 12:9 “akatupwa hata nchi”
Ø Absalomu  2 Samweli 18:15  wakamwangukia wakampiga Absalomu na kuuawa
Ø Ahithoferi 2 Sawemli 17:12  “Alijiua”
Ø Adonia 1 Wafalme 2:25 “ akampiga hata kufa”

NAMNA YA KULETA ROHO YA KUAMBATANA.
Kuna mbinu mbalimbali ambazo zaweza kutumika katika kuleta roho ya kuambatana kati ya kiongozi na washirika, baadhi ya mbinu hizo ni :-
i.                Endelea kuondoa watu wasio ambatana na kiongozi haraka.
    1koritho 5:6 “Chachu kidogo huchachua donge zima”
kama mtu anaonyesha dalili ya kuondoka na aondoke haraka akibaki anaweza
kupandikiza roho ya chuki kwa watu wengine.
Yohana 13:27 “Na baada ya hilo tonge shetani akamwingia, Basi Yesu akamwambia uyatendayo uyatende upesi”

ii.              Tengeneza moto ili kupima mioyo
     Matendo 28:3 “Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni na kuuweka motoni nyoka akatoka kwaajili ya ule moto akasongasonga mkononi”                   
Paulo aligundua alipoweka motoni   kuwa moja ya iliyoonekana kama kuni ilikuwa ni nyoka.
Ø Tengeneza wakati mgumu ili ujue moyo wa mtu
Ø Usiwe na haraka ya kuwapandisha vyeo, Mtu akiasi kwa sababu hana cheo maana yake angeasi pia baada ya kupata cheo.
Ø Jaribu kutoa uhamisho wa idara ili kupima mioyo.
Ø Fanya kazi na watu wenye nia ya kazi pekee.
Ø Tengeneza mazingira ya watu kuondoka kama wanapenda kuondoka
Ø Fundisha kwa nguvu sana kuhusu kuambatana.

2Kor 8:12 “ Maana kama nia ipo hukubaliwa kwa kadri ya alivyonavyo mtu si kwa kadri ya asivyokuwa navyo mtu”

G.  UKWELI KUHUSU KUAMBATANA
Unapotaka kuambatana na kiongozi wako ni lazima umwamini kwamba Mungu amemchagua na uamini anavyosema siyo watu wanavyosema.
a.     Yesu nae alilaumiwa
Luka 23:22 “ wakaanza kumshitaki wakisema tumemuona huyu akipotosha taifa letu na kuwazuia watu wasimpe kaisari kodi, akisema yeye mwenyewe ni Kristo mfalme”
  Yesu mwenyewe alilaumiwa kuwa,
Ø Anapotosha watu
Ø Anawaambia wasilipe kodi
Ø Anadai ni mfalme
Ø Anatoa pepo kupitia nguvu  za shetani (luka 11:15)

b.    Paulo alilaumiwa,
Matendo 24:5-6 “kwa maana tumemuona mtu huyu mkorofi, mwanzilishi wa fitina katika wayahudi wote duniani
Mathayo 12:30 “ asiye pamoja nami yu kinyume change”



H. KANUNI ZA KUAMBATANA
1.    kuambatana kwetu lazima kuwe ni kuambatana na mamlaka iliyo kuu
 1wakoritho 11:1 “mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo”

Kama unatafuta wa kuambatana naye ambatana na kiongozi mkuu daima
Warumi 13:1“ kila mtu na aitii mamlaka iliyokuu, kwa maana hakuna mamlika isiyotoka kwa mungu”

2.    Anayeambatana hawezi kuficha taarifa
Utamtambua mtu kuwa ameambatana na wewe kama atakuambia taarifa za watu waharibifu.
1Wakoritho 5:1 “ nimearifiwa habari zenu kwamba iko fitina kwenu”
Paulo alialifiwa kwamba kuna uzinzi kanisani.

1Wakoritho 1:11” nimearifiwa habari zenu kwamba iko fitina kwenu”

Esta 2:21-22 Modekai  alipata taarifa kuwa kuna mauti naye akapata taarifa”

Matendo23:12-17” Paulo alipewa taarifa na mjomba wake kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wamue Paulo.

3.    Kuambatana kuwe kimaandiko  na sio kihisia
Ø mtu akihubiri vizuri ndio uambatane nae
Ø Akiponya wagonjwa ndio uambatane nae
Ø Unaambatana na mtu ambaye Biblia inamtaja kwamba uambatane nae sio hisia au mkumbo mkumbo.
Ø Yonathani hakuambatana na  Sauli ingawa alikuwa baba yake mzazi. Aliambatana na daudi maana alijuwa kuwa huyo ndiye aliyepakwa mafuta kuwa mfalme. (1Sam 20:13)

4.    Kuambatana kuna gharama.
Ø Luka 14:26, 1Samweli 20:32-33 (Yonathani).
Ø Waebrania 11:24:26 Musa alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.





I.     MAMBO YANAYOTOKA KATIKA KINYWA CHA MTU ASIYEAMBATANA NA MCHUNGAJI.

1.    Si ni kwa unyenyekevu tu lakini wengine tunaweza kabisa kuwa wachungaji.
2.    Anakuja mgeni anamtafuta mchungaji anauliza unashida gani ?  Mgeni anajibu “nataka kumweleza mchungaji tu”   ndio maana hamponi.
3.    Mngejua niliyoonyeshwa msingeendelea na maombi.
4.    Mimi huko siji na hakuna la kunifanya. Hesabu 16:12
5.    Unaonaje jambo hili  hivi ni Biblia ?
6.    Akiwa hayupo tunakuwa huru sana.
7.     Yeye sio Mungu naye ni mtu tu.
8.    Watu wanamwogopa mimi simwogopi.
9.    Anasifia kanisa jingine.


J.     TABIA ZA MSHIRIKA MWENYE KUAMBATANA NA KIONGOZI WAKE

                   i.          Mtaje mchungaji wako mara nyingi kwenye mambo mazuri.
Kila unapofundisha, kuhubiri au unaposhauri na mifano ya miujiza ulioona  Bwana Yesu anamtumia.

                 ii.          Mnukuu kiongozi wako mara nyingi unapokuwa unaongelea mambo ya Mungu. Kanuni ni kwamba kadri unavyomwinua kiongozi wako ndivyo na wewe unainuliwa.
Yohana 12:32 “nitakapoinuliwa juu nitawavuta wote waje kwangu”

Ø  Usimnukuu kwa mambo mabaya bali mnukuu kwa mambo unayoyapenda na kuyatamani.  kila ufanyacho fanya kwa niaba ya kiongozi”
Ø  Ukitembelea, tembelea kwa niaba, sema mchungaji amenituma na anakupenda ameshindwa kuja anadharura.
Ø  Huduma au kanisa linatakiwa kuwa na kichwa kimoja tu ambacho ni Yesu na mwakilishi wake ni mchungaji, hivyo usipoenda kwenye huduma kwa niaba ya mchungaji unatengeneza vichwa kwenye huduma, na kila chenye vichwa viwili ni JITU na sio mwili wa kristo tena.

                iii.           Mpende mchungaji wako na msifie mara zote.
Ø  Siri kubwa ya kupata upako ni kuwapenda na kuwaongelea vyema wenye upako.
Ø  Kama unawapenda sana viongozi wengine na huduma zingine na humpendi na kumsifia wa kwako, fahamu kuwa hauko mahali sahihi.
                iv.          Mkaribishe mchungaji wako kwa namna ya (kumsifia) kuvutia. Vipongeze na kuvisifia vitu alivyokufundisha na vikakugusa .
Ø  Anaporudi toka safari tangaza  kwa furaha na kwa mvuto mkubwa.
Ø  Nifuraha yetu kubwa kumwona baba yetu”

                  v.          Usiwe kituo cha kupoke malalamiko na manung’uniko.
Ø  Wafanye watu wafahamu ikiwa wanataka kusengenya au kumsema mchungaji basi sio kwenye sikio lako
Ø  Kama sikio lako ni kituo basi wewe ni Absalomu wa sasa.
Ø  Unaonaje ukimkuta mtu anamsema baba yako au mama yako mzazi je utafurahia ? Mchungaji wako ni mzazi wako wa  kiroho. Mithali 30:17.

                vi.          Toa maelekezo mazuri wakati wa dharula.  Kwa mfano anapochelewa.
Ø  Mtu anayeambatana anamtetea kiongozi wake kwa gharama yoyote ile    1Samweli 18:1- 3   Wewe ni wathamani kuliko watu elfu kumi  mlinde kiongozi kwa uwezo wako wote.
              vii.           Inapotokea kwamba mchungaji wako ameshindwa kufika kwenye sherehe au popote wajulishe kwamba alikuwa anapenda kuwepo lakini kuna jambo lisilozuilika limemfanya  asije.
            viii.          Kama wewe ni mzee kiongozi siku zote wakumbushe washirika kwamba wewe sio mchungaji ila ni mzee tu.
Yohana 3:28  Ninyi wenyewe mwanishuhudia kuwa nalisema  mimi siye Kristo, bali nimetumwa mbele yake”

Yohana alipoulizwa wewe ndiwe kristo akasema mimi siye “kama unasikia ugumu na hufurahi kuwaambia watu kuwa kuna mtu aliye juu yangu ambaye ndiye baba yangu, ujue unayoshida au tatizo.

                ix.          Kiongozi, msaidizi aliyeambatana vizuri huwaambia washirika wanaomshukuru kuwa nayeye amejifunza kutoka mahali fulani.Yesu aliwaambia watu kuwa ukimwona mwana umemwona  baba.
Yohana 5:19 “ mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona baba anatenda kwa maana yote ayatendayo yeye ndiyo ayatendayo mwana vilevile

                  x.          Unapohudumia popote ni vizuri washirika wajue kuwa unafanya kwa niaba ya kiongozi wako wala si kwa niaba yako mwenyewe.

                xi.          Tunaposema kwa jina la Yesu hiyo hufanya watu waone kuwa tunafanya kwa niaba ya Yesu na hii humpa heshima Yesu. Furahi kabisa kutoka ndani unapoona mchungaji wako anainuliwa
Yohana 3:30 “Basi hii furaha yangu imetimia yeye hanabudi kuzidi bali mimi kupungua”

              xii.          Hakikisha kuwa kila kitu kinaendelea vizuri kwa mchungaji wako.Anapendwa,anaheshimiwa na yuko salama.
            xiii.          Ufurahi ukiona kiongozi wako ameingia mahali, iwe sherehe au msiba.
Kama haufurahi ujue roho  ya uasi inaanza kukutafuna taratibu.
             xiv.          Mheshimu mke au mme wa mchungaji, mtumikie au kama unazawadi mpe.
Mtu anaempokea mke au mme wa mchungaji amempokea mchungaji na anaemdharau amemdharau mchungaji.

               xv.           Uwe na muda   wa kuongea na mchungaji wako, ni muda wa kujifunza.
Jifunze kitu  kutoka kwake siku zote.
Ø  Usione tabu kuwa karibu na mchungaji, jifunze vitu vipya.

             xvi.          Chukua mafundisho ya mchungaji wako kama yako. Mfano kanda, vitabu, CD/DVD

           xvii.          Kwenye mahubiri yako usiache kumnukuru kiongozi wako kama mmoja wa watu waliofanikiwa kihuduma.

         xviii.          Tendea kazi maamuzi na mipango yake.
  Wazo lake zuri lakini……………….
             xix.          Usianzishe ushirika bila ruhusa.

               xx.          Kumpa mchungaji zawadi. “Mithali 18:16”

             xxi.          Kumsindikiza na kumpokea mchungaji anaposafiri.

           xxii.          Wakati wa ushauri ni vizuri kujifunza kumsaidia sawasawa. Usichangie ushauri kinyume na aliotoa mchungaji.
Ø  Usijaribu kuleta hekima nyingine yoyote.
Ø  Wewe msaidie kiongozi kwa kusisitiza anachosema.
a)     Umeelewa anachosema mchungaji ?
b)     Unaelewa anachokusaidia mchungaji ?
c)     Mchungaji anasema haya kwa sababu anakupenda.s
d)     Natamani kipindi kile nilichokuwa kwenye hali kama hii, ningepata mtu wa kunitia moyo hivi.
         xxiii.          Kiongozi anaeambatana huandika yale mchungaji anasema na kufundisha.
a)     Kuandika ni hali ya unyenyekevu.
b)     Kutoandika ni hali ya uasi.

         xxiv.          Anaeambatana yuko tayari kumtetea kiongozi wake kutokana na makosa yanayoweza kujitokeza katika shughuli za kila siku.
Ø  Hakuna asiyekosea.
Ø  Sasa ole wako ukosee halafu una watu wasioambatana na wewe.
           xxv.           Kutoa ushauri mzuri kwa mchungaji na ukikataliwa hachukii.
         xxvi.           Anaeambatana anatosheka na nafasi anayopewa.
Ø  Upako maradufu wa Elisha (2 Samweli 2:1-14)
Ø  Tahadhari (Warumi 16:17) waangalieni.



SURA YA NNE
MBINU ZA  KUWALETA WATU KWA YESU.
Tunaweza kutumia mazingira katika kuhubiri na kufundisha Neno la Mungu. Yesu alitumia mazingira katika kuhubiri Injili. Alisimulia habari zilizoendana na utamaduni wa watu kwa kutumia vitu vya kawaida vilivyopatikana katika mazingira yao.
   Alitumia mifano ya ngano, mtini, zabibu, kondoo, mnara , uvuvi na vitu vingine vingi  katika  kufundisha kweli za kiroho.
 Mazingira yalikuwa ni uwanja ambapo wanafunzi wa Yesu walifanyia kazi  kweli walizojifunza.
 Katika kipengere hiki tutaangalia vitu viwili Yesu alivyotumia katika kufundisha ambavyo ni Uvuvi wa samaki na ukulima yaani udongo.

1.    UVUVI WA WATU.
Mstari wa ufungo.
“Yesu akawaambia, njoni mnifuate, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu”. Marko 1:17
Wakati Yesu alipoanza huduma yake ya hadharani  hapa duniani aliwaita watu kadhaa ili kuwa wanafunzi wake wa awali.
Agizo(amri) lake la kwanza lilikuwa ni kujizidisha  kiroho. Kama wangemfuata, yeye  angewafanya wavuvi wa watu.Wangeanza   kuvua kiroho wanawake na wanaume kama wao.
Ujumbe wa mwisho wa Yesu kwa wanafunzi wake ulikuwa ni wito kwa uzazi na mazidisho ya kiroho.
“Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho mtakatifu; nanyi mtakuwa  mashahidi wangu katika Yerusalemu na katika Uyahudi wote na Samaria na hata mwisho wa nchi. Akiisha kusema hayo;walipokuwa wakitazama akainuliwa wingu likampkea kutoka machoni pao   Matendo ya Mitume 1:8-9

Ni  jinsi gani wanafunzi wangeweza kutimiza hili agizo kuu walilopewa na Yesu?
Namna  gani kundi hili la watu wangejizidisha na kuufikia ulimwengu wote ?

a.    Mbinu za mazidisho.
Yesu alifunua mbinu maalumu ambazo zingewawezesha wanafunzi wake kutimiza agizo kuu. “Kuzaa Kiroho” Mojawapo na muhimu ya mbinu hizi zilitolewa kama sehemu ya Agizo kuu katika Matendo ya Mtume 1:8.
Wanafunzi wangejizidisha kupitia  kuvikwa nguvu na Roho Mtakatifu.Mbinu zingine zilifunuliwa pale wanafunzi walipoanza kujizidisha na kuufikia ulimwengu kwa Injili.  Mbinu hizi zimeandikwa katika kitabu cha Matendo ya mitume. Na nyaraka katika Agano jipya.
Mada inalenga kutoa ufafanuzi wa hizi mbinu za  mazidisho.  Somo hili linakufundisha wewe jinsi ya kutumia mbinu hizi ili kuweza kujizidisha kiroho na kuweza kutimiza Agizo kuu la Mungu.
Lakini kabla ya yote unapaswa kuelewa maana ya kujizidisha.
Kuzidisha ni kuongezeka mara nyingi  kiidadi kwa  kujizidisha.Kitu kinapojizidisha huzaa zaidi na zaidi katika ufanano uleule.Mazidisho ni matokeo ya kuzidisha.
Mfano 3×3 = 9, wakati 3+3 =6.  4×3 maana yake ni kwamba  namba 4 zinatakiwa kuwa tatu, yaani 4, 4, 4 ambako huleta jawabu la 12. Hivyo kuzidisha huleta jawabu kubwa kuliko kuongeza. Jambo la msingi hapa ni kwamba namba moja hujirudia mara kadhaa  katika mfanano ule.
Katika ulimwengu wa asili wanawake na wanaume wanazaliana wenyewe  kwa kuwa na watoto. Wanajizidisha kimwili.
Mazidisho ya kiroho yanatokana na kuzaliana kiroho. Mwamini huzaa kiroho kwa kuwashirikisha  Injili watu wengine wasiomjua Mungu (wasiookoka)  kwa kushuhudia na kuhubiri na kuwaongoza hao aliowashuhudia au kuwahubiri kuwa waamini na kuwawezesha kuwa wanafunzi wa Yesu.
Biblia inadhihirisha mbinu za ki Mungu kwaajili ya mazidisho ya  kiroho.
Mbinu ni mpango uliowekwa kwajili ya kufanikisha lengo fulani mahususi. Au ni hatua zinazowezesha jambo fulani kufanyika kwa ufanisi kama ilivyokusudiwa.
 .
Lengo halibadilikji.  Tunatakiwa kuzaa kiroho na kuufikia ulimwengu wote kwa Injili  ya Yesu Kristo.  Kuna mbinu mbalimbali ambazo kwazo lengo hili laweza kifikiwa .  Mbinu hizi kwa pamoja huitwa methodolojia ya mazidisho.
Wakati Mwamini anafanyia  kazi mbinu za ki Mungu za mazidisho matokeo yake huwa ni uzao wa kiroho.Yaani waamini wapya huzaliwa kiroho katika mji wa mimba ambao ni kanisa.

b.    Wito kwa matendo
Watu ambao  Yesu aliwaita kwanza kuwa wanafunzi wake  walikuwa ni wavuvi.Walikuwa ni watu wenye kazi. Hawakukamata   samaki kwa wakati mmoja. Walitumia nguvu kubwa kuvua na kupata samaki wengi wa kila aina.
Wakati Yesu alipowaita kuwa wavuvi wa watu alidhihirisha mpango  wenye kufanana na ile kazi yao ya uvuvi  kwaajili ya mazidisho ya kiroho. Wanafunzi wake walitakiwa kuvua watu toka kila taifa, tamaduni, lugha na makabila yote. Nyavu zao za kiroho zingejazwa.
Yesu aliwaita watu kwaajili ya  kazi .Alisema angewafanya kuwa wavuvi wa watu.Hawangekuwa  watazamaji  tu  katika mpango wa Mungu.Wangekuwa washiriki   wakuu kwa kuwa wavuvi  wa roho za watu.Wito wa Yesu bado ni sawa. Haujabadilika.Tunapaswa kuwa wavuvi wa watu.  Kama si wavuvi basi si wanafunzi.
c.     Wavuvi wa watu
Kwanini Yesu alitumia mfano wa uvuvi kuwaita wanafunzi   wake ?
Kwanza ulikuwa ni mfano ambao wangeuelewa  kwa urahisi.Hawa watu waliishi  kwa shughuli ya uvuvi. Kazi ya uvuvi ilikuwa ni kitu ambacho walitumia nguvu zao nyingi na muda wao mwingi. Wakati Yesu alipowaita kuwa wavuvi walielewa  kwamba wangewavua  samaki (watu) katika ulimwengu wa kiroho.
Walielewa pia mahitaji ya wito huo.  Uvuvi wa kiroho ungehitaji kujitoa kikamilifu.  Kutoa muda na nguvu.
Pili Yesu alitumia mfano wa uvuvi kuwaita wanafunzi wake kwa sababu kuna kanuni za uvuvi wa asili  zinazoweza kutumika katika uvuvi wa watu (uvuvi wa kiroho).
Baadhi ya kanuni hizo ni:
1.    Unapaswa kwenda mahali samaki walipo.Kama unataka kupata samaki unapaswa kwenda samaki walipo.  Samaki huishi majini.  Huwezi kuwapata samaki kwa kuwasubiri ukiwa juu ya mlima au ukiwa jangwani.  Mvuvi wa watu unapaswa kwenda mahali ambako watu ambao hawajaokoka wanapatikana au kuishi.  Watu ambao hawajaokoka wanapatikana katikia maeneo mbalimblai huwezi kuwasubiri katika mejengo ya kanisa ndipo uwavue. Nenda mahali wanakopatikana,  mfano sokoni,mashuleni, hospitalini, magerezani,maofisini majumbani na mahali pengine popote wanakopatikana na kisha wavue

2. Lazima uchunguze  mazingira.  Katika uvuvi wa asili mvuvi anapovua huzingatia mazingira, huchunguza kina cha maji, aina ya maji, ili kujua kama ni maji ya chunvi au la, namna upepo unavyopiga. Mambo haya yote kwa kawaida hutoa tathimini ya  aina ya mtego na mbinu  unazopaswa kutumia Kuvua.  Hizi pia ni mbinu utakazotumia katika uvuvi wa watu.  Kweli hizo hapo juu ni sawa kabisa katika mambo ya kiroho.  Nilazima uchunguze  mazingira ambamo watu wanaishi.  Nini mahitaji yao?  (Tambua mahitaji yao) Nini kinaendelea katika maisha yao?   Hii itakusaidia wewe  kujua mbinu utakazotumia  katika kuwavua watu hawa.
Yesu alipokutana na mwanamke kisimani katika Injili  ya Yohana 4 alichunguza mazingira aliyomkuta  yule mwanamke .  Alikuwa anatafuta maji ya kawaida.  Yesu alitumia hitaji hili la mwanamke  kumsaidia kutambua hitaji lake la kiroho. Mbinu aliyotumia   ilimleta mwanamke katika ufalme wa Mungu.
 Kama huchunguzi mazingira katika uvuvi  wa kiroho (watu) utajikuta mwenyewe unavua juu ya mlima.  Kwa sababu hujui watu wanakopatikana na jinsi ya kuwafikia.
3      .Tumia mbinu mbalimbali. Mvuvi bora hutumia mbinu mbalimbali katika kuwakamata  samaki.  Hutumia vitu mbalimbali ili kuwavutia samaki. Hutumia zana mbalimbali za uvuvi . Aina mbalimbali za samaki huvutiwa na mbinu mbalimbali za uvuvi.  Ndiyo maana mvuvi bora hutumia mbinu mbalimbali. Mvuvi aweza kujifunza baadhi ya mbinu hizo katika vitabu vinavyohusu uvuvi. Anajifunza mbinu zingine kutokana na uzoefu na uchunguzi wa kina. Mbinu anazotumia hubadilika lakini lengo daima linabaki kuwa lilelile. Kukamata samaki.
Kama unataka kuwa mvuvi bora wa watu unapaswa kutumia mbinu mbalimbali. Watu  wanatofautiana hivyo hata vitu vinavyowavutia vinatofautiana. Wengine huvutiwa na mahubiri au mafundisho aukufarijiwa wakati wa matatizo. n.k. Mbinu za uvuvi wa kiroho zinatofautiana lakini lengo daima ni lilelile. Kupata roho zilizopotea na kuzileta kwa Yesu Kristo.

4. Unapaswa kutoa nje na kurudisha tena. Haijalishi mbinu unayotumia, unapswa kuitupa nyavu majini na kuitoa tena.  Katika uvuvi wa kawaida  jinsi unavyotega mitego yako majini ni jambo muhimu sana. Unatakiwa kutega mitego yako kwa umakini sana . Pia unapaswa kuwa makini katika kuwatoa samaki kwenye mitego baada ya kuwakamata.
Katika ulimwengu wa roho tumeahidiwa kwamba tukilitoa Neno la Mungu halitaturudia bure. Litafanikisha  lengo katika maisha ya watu Isaya 55:11.
Unapotumia Neno la Mungu utakuwa katika shabaha kila wakati na hatimae litawakamata wanawake na wanaume nakuwaleta katika ufame wa Mungu.

5. Tambua majira na nyakati.Majira ma  nyakati huathiri sana shughuli ya uvuvi katika ulimwengu wa asili. Baadhi ya samaki huhama na hawawezi kupatikana katika baadhi ya kanda wakati wa majira fulani.  Samaki wakubwa hukamatwa mapema mchana wanapokuja katika eneo la juu la uso wa maji ili kupata chakula.  Kama utavua katika majira yasiyo sahihi au muda usio sahihi huwezi kuwakamata samaki wengi. Wakati ni muhimu sana katika uvuvi wa kiroho pia.

6.  Lazima uwe mvumilivu.Katika ulimwengu wa asili mvuvi hutakiwa kuwa mvumilivu. Ni lazima asubiri samaki waingie kwenye mtego aliotega na kukamatwa.  Hii pia ni kweli katika ulimwengu wa roho.
Kwahiyo ndugu vumilieni hata kuja kwake Bwana. Tazama mkulima hungoja mazao yake ya nchi  yaliyoyathamani, huvumilia kwaajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho  Yakobo 5:7.


C. Kuzaa kiroho
Katika ulimwengu wa asili samaki hupelekea kutokea kwa samaki wengine wengi kwa njia ya kuzaliana. Uvuvi katika ulimwengu wa asili husababisha mazidisho ya samaki .
Uvuvi katika ulimwengu wa  roho husababisha mazidisho  ya watu katika ufalme wa Mungu. Uzazi wa kawaida husabisha mazidisho ya watu walio hai. Uzazi wa kiroho husababisha  pia mazidisho ya watu walio hai kiroho.
Hii haiji kutokana na programu  za kibinadamu.  Uzazi wa kiroho huja kupitia mtiririko wa maisha ya kiroho toka kwa Mungu. Katika maisha ya kawaida ya binadamu maisha ya kiumbe kipya  huanza  katika tumbo la uzazi la mwanamke(uterus) na seli hai moja . Seli hiyo  hujizidisha hadi mtu kamili anapokuwa amefanyika.  kisha mtoto huzaliwa.
Uzazi wa kiroho pia ni sawa na huo.Huanza na mtiririko wamaisha  ya ki-Mungu kwa mtu mmoja , hujizidisha katika tumbo la kiroho la uzazi  ambalo ni kanisa nakisha mtoto wa kiroho huzaliwa.


2.  UDONGO.
Andiko:  Mathayo 13:3-9, 18-23
Yesu alitoa mifano mingi iliyohusu  kilimo. alizungumzia habari za mpanzi, habari ya wakulima. N.k
Kutambua udongo wa kiroho wenye mbolea. Katika ulimwengu wa kawaida wakulima huchunguza udongo kwanza kabla ya kupanda mazao yao kwa sababu kuu tatu ambazo ni :-
 Sababu ya kwanza:- Wanataka kuchagua udongo bora kabisa ambako wataelekeza nguvu zao zote. Wanajua kwamba udongo wenye mbolea  ya kutosha  ndio utakao leta mazao mengi.

Sababu ya pili: Kutambua udongo  duni ili waweze kujua namna ya kuuandaa kwa kilimo. Waweze kutambua namna udongo huo unavyoweza kuboreshwa na kufaa kwa kilimo.


Sababu ya tatu: Kutambua udongo ili kujua mbinu  zinazotakiwa kutumika katika kilimo.
Kutambua kwamba kama itahitaji kutumia kilimo cha umwagiliaji, aina ya mazao yanayotakiwa kupandwa na namna ya uvunaji mazao.

Utafiti wa mazngira  katika ulimwengu wa roho unafanana na kile wakulima wanachofanya katika  ulimwengu   huu. Tunawachunguza, watu,  na maeneo kwa sababu tatu ambazo ni:-
i.                  Tunataka kujua eneo lenye mbolea zaidi kiroho.
 Baadhi ya maeneo yako tayari kwa mavuno ya kiroho. Biblia inasema kwamba watendakazi ni wachache katika uwanja wa mavuno, hivyo tunataka kujikita  katika maeneo ambayo yako tayari kwa uvunaji.Lengo letu kuu ni kutoa kipaumbele kkwa maeneo yaliyo tayari kwa mavuno.
ii.               Kutambua mbinu tunazoweza kutumia kufanya ili eneo lisilofaa liweze kufaa kwa mavuno ya kiroho. Kuna baadhi ya maeneo ambayo hayako tayari kuipokea Injili, Maeneo hayo ni sawa na udongo usio na rutuba yanahitaji mikakati maalumu ili yaweze kufaa kwa mavuno ya kiroho.

iii.             Ili kutambua mbinu nzuri zaidi za kiuinjilisti na umisheni zenye kuleta matokeo makubwa katika  kuwaleta watu kwa mwokozi.